• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Upanuzi Barabara Kukamilika Mei

Posted on: March 20th, 2018


Utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa barabara ya Makongoro hadi uwanja wa ndege unatarajia kukamilika mei 2 mwaka huu.

Mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo uliosainiwa April 18 mwaka 2017 na M/s Nyanza Road Work Ltd ambapo gharama za mradi ni shilingi 9,542,701,531.96 unaosimamiwa na kitengo cha ushauri wa kihandisi cha wakala wa barabara TECU.

Akizungumza kwenye kikao cha pili cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mwanza kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mwanza Mhandisi Marwa Rubirya kilichofanyika jana mkoani hapa alisema, hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 74 ambapo ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Mwaloni-Furahisha na Pasiansi hadi uwanja wa ndege upo katika hatua mbalimbali.

Mhandisi Rubirya alisema, uwekaji wa tabaka la lami ngumu imefikia urefu wa km 2.2, lami ya awali urefu wa km 2,9, tabaka la mawe yaliyosagwa urefu wa km 2.9,tabaka la msingi wa barabara km 3.1 na ujenzi wa daraja la Ilemela umekamilika kwa asilimia 90, hivyo utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kukamilika mei 2 mwaka huu.

Hata hivyo alisema, usanifu wa kina wa upanuzi wa daraja la Mabatini lililopo barabara ya Mwanza- Musoma utakamilika mwezi aprili mwaka huu na kazi inaendelea inayofanywa na Mkandarasi Mshauri M/s Advance Engineering Solution kwa gharama ya milioni 242,574.

Hatua hii ni kutokana na kuepo tatizo la mafuriko kwa muda mrefu kwenye daraja hilo pindi mvua zinaponyesha na kusababisha maji kupita juu ya barabara kwa kuwa na midomo midogo ya kupitishia maji.

Aidha, ofisi ya Meneja mkoa kwa kushirikiana na wahandisi washauri wataendelea kusimamia utekelezaji wa miradi yote ili ikamilike kwa wakati kama ilivyopangwa hivyo kwa kuiwezesha ofisi yao kutekeleza majukumu ya kujenga na kusimamia matengenezo ya barabara kama ilivyoidhinishwa katika bajeti ya wizara yao wanashauri fedha zitolewe kwa wakati.

Kwa upande wake Mratibu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Mwanza Francisco Magoti alisema, dhima yao ni kupanga,usanifu,ujenzi, ukarabati na matengenezo ya mtandao wa barabara za vijijini na mijini kwa kuzingatia ufanisi wa gharama kwa ajili ya maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi nchini.

Alisema, TARURA ina mtandao wa barabara wenye urefu wa km 4891.56 kwa Halmashauri zote za mkoa huo,ambapo barabara ya lami km120.41,barabara ya mawe km 8.537, barabara ya zege km 2.51, barabara za changarawe km 1525,673 na barabara ya udongo km 3235,22.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela John Wanga aliomba kipande kitakacho baki cha barabara ya Buswelu hadi Igoma nacho kijengwe kwa kiwango cha lami, ili kuleta taswira nzuri na wananchi kufanya shughuli za uchumi kwa urahisi baada ya kukamilika kwa mradi wa barabara ya Buswelu kupitia Kiseke mpaka Sabasaba ambao unakaribia kuanza mei, huku Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mary Tesha aliwaomba TARURA kuendelea kushirikiana na wakuu wa wilaya na wabunge katika kutekeleza majukumu yao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti