• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

VIJANA MWANZA WAASWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Posted on: March 29th, 2025

VIJANA MWANZA WAASWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI


Serikali Mkoani Mwanza imewataka Vijana wa Mkoa huo kuchangamkia fursa mbalimbali ili waweze kupata kipato kitakachowasaidia kujikwamua na umaskini pamoja na kuboresha hali ya maisha.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Machi 29, 2025 alipokuwa akizungumza na Vijana walioshiriki katika Kongamano la PPRA linalohusu Fursa za Kiuchumi Mkoani Mwanza.

Mkuu wa Mkoa amesema Serikali ya awamu ya sita imeweka mazingira mazuri ya kuimarisha vipato vya wananchi wote kupitia Mifuko ya Maendeleo kwa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu ambapo kwa sasa dirisha la mikopo limefungwa tangu Oktoba, 2024.

Aidha Mhe. Mtanda amesema Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023, imezitaka Taasisi zote za Serikali kutenga Asilimia Thelathini ya bajeti zake kwa ajili ya Makundi Maalum (Wanawake, Vijana, Wazee na Watu Wenye Ulemavu).

“Kiasi hiki ni kwa ajili ya Watanzania ambao wanaweza kujikusanya na kuunda vikundi rasmi vya vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu, kisha washiriki kwenye tenda za Serikali”.

Ninawasihi sana, mfuatilie kwa makini taarifa mtakazopewa katika Kongamano hili, ili mfahamu jinsi ya kupata sehemu ya fedha hizi kupitia Mfumo wa NeST, na kujiinua kiuchumi. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Naye Mkurugenzi wa Generation Samia, ambaye pia ndiye mratibu wa kongamano hilo Bw. Omary Kimweri amesema wao kama Kizazi cha mfanikio au maarufu kama Generation Samia wamedhamiria kuyaunganisha makundi mbalimbali na fursa zinazotengenezwa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Ndugu Dennis Simba, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) amesema fedha hizo 30% Serikali ya Dkt. Samia sio fedha chache ni nyingi sana ambapo ni zaidi ya trilioni 5 kwa bajeti ya mwaka mzima

Kadhalika ameahidi kuendelea kutoa elimu ili makundi hayo yaweze kujipanga kwa kutafuta fursa mbalimbali na amesema mpaka leo ni takribani trilioni 15 zimekwisha tolewa tangu kuanza kwa sheria hiyo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti