• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WACHEZAJI WA PAMBA JIJI FC WAOGA NOTI, RC MTANDA AWAPA SOMO WAAMUZI

Posted on: February 10th, 2025

WACHEZAJI WA PAMBA JIJI FC WAOGA NOTI, RC MTANDA AWAPA SOMO WAAMUZI


Wachezaji wa timu ya soka ya Pamba Jiji FC wameoga noti shilingi milioni 15 na kuahidiwa nyongeza nyingine kama hiyo ndani ya siku chache kama muendelezo wa motisha huku Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda akiwakumbusha waamuzi kuzingatia sheria 17 za mchezo wa soka.

Katika hafla fupi ya kuwakabidhi fedha hizo iliyofanyika leo Februari 10,2025 kwenye uwanja wa michezo wa shule ya Sekondari Lake, RC Mtanda amebainisha  kuwa soka ni mchezo wa burudani na amani lakini akitokea mwamuzi na tafsiri tofauti atasababisha jazba na vurugu.

"Rai yangu kwa waamuzi, sasa hivi ligi kuu ipo hatua ya lala salama waamuzi wadumishe amani michezoni kwa kuchezesha kwa haki dimbani, mashabiki wanapenda burudani na siyo vinginevyo”. amesisitiza Mhe. Mtanda ambaye pia ni mlezi wa timu ya Pamba Jiji.

Katika hafla hiyo Mkuu huyo wa Mkoa amefafanua kila ushindi kwa timu za uzito wa juu kama Simba, Yanga na Azam motisha itakuwa shilingi milioni 15 huku Ile walivyokubaliana na uongozi kwa timu nyingine ushindi motisha ni shs milioni 10.

"Nimeahidi kwa ushindi dhidi ya Azam tutawapa shs milioni 15 lakini kuna baadhi ya wadau wa soka wa Mkoa wetu wamefurahishwa na mwendo mzuri wa timu na kuniunga mkono kwa kunichangia fedha, sasa baada ya siku chache nitawakabidhi shs milioni 15 nyingine na kufanya jumla iwe milioni 30”. Mhe. Mtanda.

Mfungaji wa bao la ushindi mchezaji Deus Kaseke amekabidhiwa kitita cha sh. laki saba na nusu, mfungaji wa bao lililokataliwa Salehe Masoud ameondoka na kibunda cha laki mbili na nusu, mchezaji aliyetoa pasi iliyozaa bao la ushindi Yonta Camara amepata sh. laki moja pamoja na mlinda mlango Yona Amos amekabidhiwa laki moja kwa muendelezo wa kutoruhusu nyavu zake kutikiswa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewaomba wale wadau wenye nia njema na Pamba Jiji walete michango yao kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa au Mkurugenzi wa Jiji ili kuzidi kuwapa motisha wachezaji wa timu hiyo ambayo Jumamosi hii watawakaribisha Coastal Union kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

Pamba Jiji FC maarufu kama TP Lindanda Wana Kawekamo baada ya ushindi dhidi ya Azam FC imechumpa hadi nafasi ya 12 na mtaji wa pointing 18 kibindoni katika msimamo wa ligi kuu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti