• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAELIMISHAJI JAMII MWANZA WANOLEWA USAFIRI WA M-MAMA

Posted on: July 12th, 2024

WAELIMISHAJI JAMII MWANZA WANOLEWA USAFIRI WA M-MAMA


Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba leo Julai 12, 2024 amefungua kikao kazi cha kuwajengea uwezo Waelimishaji jamii ngazi ya Mkoa na Halmashauri kuhusu usafiri wa dharula kwa Mama na Mtoto Mchanga (M-MAMA) chini ya ufadhili wa Pathfinder.

Akifungua kikao hicho Dkt. Lebba amewataka waratibu wa afya ya Mama na Mtoto, waratibu wa elimu ya afya kwa umma na waratibu wa mradi wa M- Mama kupeleka fedha kwenye akaunti ya Taifa ya M-Mama ili kufanikisha utekelezaji wa malengo kibajeti na akasisitiza kutochelewesha malipo.

"Hakuna kitu kinanikera kama kuona kifo cha mama na mtoto katika kazi zangu, pamoja na makusanyo bora ya mapato ya ndani kutokana na huduma za afya kipaumbele changu kingine ni kuona hakuna vifo vya mama na mtoto, naomba tushirikiane kufanikisha haya," amesisitiza Mganga Mkuu.

Aidha, amewataka wataalamu hao kuhamasisha jamii kuweza kutumia huduma hiyo kwa manufaa hususani matumizi sahihi ya namba ya dharula 115 kwa jamii ili isitumike vibaya badala yake waitumie kwa ajili ya kuomba msaada tu pale unapohitajika usafiri kwa mama au mtoto mchanga.

Vilevile, amesisitiza umuhimu wa kutoa mrejesho wa utekelezaji wa mpango kazi na katika hilo amewataka kufuata sheria, kanuni na taratibu za afya ikiwemo na utoaji huduma bora kwa wananchi na kwa staha ili kujenga imani kwa jamii dhidi ya Serikali juu ya huduma za afya hususani zilivyoboreshwa.

Wakati akiwasilisha mada, mwezeshaji kutoka Hospitali ya Mkoa wa Arusha (Mount Meru) Bi. Shubila Mujwahuzi alibainisha malengo ya mradi huo kuwa ni kupunguza vifo vya wajawazito na watoto ili kuimarisha rufaa kwa kuanzisha pia vyumba maalumu wagonjwa wa dharula.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti