• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO MWANZA WAHIMIZWA KUIMARISHA NIDHAMU ILI KUKUA KIUENDELEVU

Posted on: September 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wafanyabiashara ndogondogo mkoani humo kuwa na nidhamu ya shughuli zao ili kuendeleza  mitaji na kupata faida zenye tija.

Ametoa wito huo leo Septemba 02, 2025 wakati akihutubia katika kongamano la wafanyabiashara ndogo ndogo wa Mkoa huo lililowakutanisha makundi mbalimbali wakiewemo Machinga, Maafisa Usafirishaji (Bodaboda & Bajaji), Wasusi, Washonaji, Mama Lishe, Baba Lishe na waendesha Guta.

Mhe. Mtanda amesema biashara inahitaji kujielimisha hususani masuala ya mitandao ili kujua ni taasisi gani inatoa hifadhi ya jamii na waweze kujiunga pamoja na kujihakikishia ulinzi wa mitaji kwa kujisajili kwenye bima kama za moto na ajali.

Aidha, amewapongeza wajumbe wa kongamano hilo kwa kupata elimu ya masuala mbalimbali hususani kuzifahamu taasisi za kifedha zinazokopesha mitaji na akatoa wito kuzingatia elimu iliyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima nchini (TIRA) ili kulinda biashara zao.

“Mtembea bure sio sawa na mkaa bure, mmejifunza mengi na nawapongeza waandaaji wa kongamano hili kwa kugusa kila rika na kundi kuhakikisha wanawajengea uwezo katika masuala mbalimbali, nendeni mkayafanyie kazi na kuwafikishia wengine elimu mliyopata.” RC Mtanda.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwaalika kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025 kwa kuanza kushiriki kwenye kampeni na uchaguzi wenyewe kwa amani na utulivu.

Akisoma risala ya wafanyabiashara ndogondogo Ndugu Aziz Jabir ametumia jukwaa hilo kutoa shukrani kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea ofisi katika Mikoa yote na kuwaletea vitambulisho vinavyowafanya watambulike na kupewa mikopo na taasisi za kifedha kote nchini.

Aidha, ameipongeza serikali kwa kuchochea shughuli zao kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara, Maji, Bandari, Reli na Vivuko nchini na akabainisha changamoto ya usajiri unaolegalega kwani ni wafanyabiashara elfu 2 pekee kati ya zaidi ya elfu 6 waliopo Mwanza ndio wamesajiriwa na kukwamisha ukopaji wa fedha za mitaji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti