• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAFUGAJI MWANZA WATAKIWA KUFUGA KISASA KUKIDHI MAHITAJI SOKO LA NYAMA KIMATAIFA

Posted on: September 2nd, 2024

WAFUGAJI MWANZA WATAKIWA KUFUGA KISASA KUKIDHI MAHITAJI SOKO LA NYAMA KIMATAIFA


Mkuu wa mkoa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wafugaji Mkoani humo kuachana na ufugaji wa kienyeji wa mazoea na kufuga kisasa mifugo yao ili wakidhi mahitaji ya soko la nyama kimataifa.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo Septemba 2.2024 alipotembelea kiwanda cha nyama cha Chobo Investment kilichopo wilayani Misungwi kujionea uzalishaji na uchakataji nyama unaofanywa na kiwanda hicho.

Amesema nchi yetu ina zaidi ya ng'ombe Milioni 40 na inashika nafasi ya pili kwa ufugaji ng'ombe ikitanguliwa na Ethiopia lakini ni asilimia 5 tu ya mifugo hiyo ndio wanafaa kwa uzalishaji nyama hiyo, hali inayopelekea pia kutokufanya vizuri katika uchangiaji wa pato la Taifa ambapo kwa sasa ufugaji unachangia kwa asilimia 7 tu.

Aidha, amempongeza mwekezaji huyo kwa kupanua kiwanda hicho kwa dola za kimarekani milioni 3 zaidi kutoka kwenye 10 za awali zilizolenga kuongeza uchakataji wa mazao ya nyama kutoka matumizi ya 47% hadi 100% na kwamba itasaidia pia kupatikana kwa bidhaa 153 zinazotokana na mfugo ng'ombe.

Naye, Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bw. John Chobo amesema kiwanda chao kina uwezo wa kuchinja ng'ombe 600 kwa saa 8 lakini kwa sasa wanachinja 200 tu huku wakipata mbuzi wachache kutokana na uzalishaji kuwa wa kiwango cha chini na usiokidhi mahitaji.

Amefafanua kuwa ili kufikia malengo ya kupata nyama ya kutosha wameanzisha shamba ambalo wanafuga kisasa, wananenepesha na kuandaa malisho bora kwa mifugo na akatumia wasaa huo kuwakaribisha wafugaji kwenda kujifunza ili wazalishe kisasa.

"Kiwanda chetu ni kikubwa na tumekiongezea nguvu hivyo tunatamani kupata ng'ombe wenye uzito mkubwa hadi wa Kilogram 700 kwani mahitaji ya nyama kwenye soko la ndani na nje ni makubwa sana lakini kunakua na uhaba kutokana na ng'ombe wa asili kuwa na uzito mdogo." Amesema Bwana Chobo.

Vilevile, ametoa wito kwa sekta ya kilimo kuchangia kwenye ukuaji wa nyama kwa kuzalisha vifungashio vitokanavyo na zao la pamba linalofanya vizuri nchini (Mutton Cloth) vinavyotumika kuhifadhi nyama kwenda nje ya nchi tofauti na hali ya sasa ambapo vinaagizwa kutoka Vietnam.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti