• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAGONJWA KIPINDUPINDU MWANZA WAPUNGUA-RC MAKALLA

Posted on: January 24th, 2024

WAGONJWA KIPINDUPINDU MWANZA WAPUNGUA-RC MAKALLA


*Asema kuna mpya 1 na waliolazwa 7 tu Mkoani Mwanza*


*Awataka TARURA kuondoa maji yaliyotuama kwenye mitaro*


*Asema kwenye mikusanyiko tuzingatie usafi na kanuni za afya kutokomeza Kipindupindu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema Maambukizi ya ugonjwa wa Kipindupindu Mkoani yamepungua sana kwani kuna mgonjwa mpya mmoja tu ambapo saba pekee wakiwa hospitali wamelazwa kwenye maeneo mbalimbali na akawataka wadau kuendelea na mikakati ya kuthibiti kusambaa.

Mhe. Makalla amebainisha hayo mapema leo Januari 24, 2024 wakati wa mkutano wake na Mganga Mkuu wa Serikali,Prof.Tumaini Nagu uliofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huku ukiwakutanisha viongozi wa Taasisi mbalimbali za Serikali za Mkoa huo.


Makalla amesema ni lazima kuendelea na mikakati ya kuthibiti kusambaa kwa maradhi hayo huku akitaja afua ya kuzibua mitaro ili maji ya mvua yasituame na kufikia hatua ya kusambaa kwenye makazi ya watu.

Akibainisha namna tatizo hilo lilivyo dhahiri Makalla amesema tangu kuibuka kwa ugonjwa huo juhudi mbalimbali zimefanywa kuudhibiti na akatumia wasaa huo kukemea tabia ya kuishi kwa mazoea hususani kwenye tabia za ulaji wa vyakula bila kuosha hasa Matunda.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu amewataka wadau wa afya na viongozi wengine kuzingatia sheria ndogondogo za Serikali za mitaa ili kuhakikisha afya ya jamii inazingatiwa hususani kwenye makundi kama ya mialo ya uvuvi.

"Ukiugua kipindupindu maana yake umekula mavi mabichi, aidha kwa uchafu kupitia kula kinyesi chenyewe au kupitia vitu mbalimbali tunavyoweka mdomoni kwa mikono isiyo safi, hivyo ni lazima watu wanawe mikono kwa maji safi na salama tena kwa Sabuni wakati wote" Prof. Nagu.

Halikadhalika, Mganga Mkuu ametoa wito kwa jamii kula vyakula vya moto, kuosha matunda na kunawa mikono kwa naji safi na salama yanayotiririka na kwa sabuni ili kukomesha kabisa janga hilo ndani ya Mkoa na ukanda huo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti