• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wahandisi na Maafisa ugavi wa Halmashauri wapewa Rai kuwa na weledi mradi wa BOOST

Posted on: May 4th, 2023


Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Martin Nkwabi amewataka Wahandisi na Maafisa Ugavi wa Halmashauri kuwa waadilifu na kutekeleza Mradi wa BOOST kwa wakati na ufanisi.  

Bwana Nkwabi ametoa kauli hiyo mapema leo tarehe 03.05.20223 Jijini Mwanza wakati akifungua Mafunzo ya kuwajengea uwezo Wahandisi na Maafisa Ugavi wa Halmashauri kuwa waadilifu na kutekeleza Mradi wa BOOST kwa wakati na ufanisi.  

“kuna shida ya kimaadili ambayo wakati fulani inatufanya tuachane na utaalamu wa fani tulinayo, nisisitize umuhimu wa uadilifu na kuzuia mmomonyoko wa maadili katika utendaji kazi wetu, ninyi ni watumishi wa Umma msikwame kwenye tope la maadili” amesema Nkwabi.

Aidha, amewataka Maafisa hao kuzingatia vipaumbele na malengo ya Mradi huo wa Sekta ya Elimu ili kuondoa hoja za ukaguzi na kuukamilisha Mradi chini ya viwango stahiki kwani kwa kufanya hivyo kunaipotezea Serikali fedha nyingi ikiwa ni pamoja na kupata fedha za Wahisani.

Akiongea kabla ya mgeni rasmi, Joel Mhoja Mratibu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema Maafisa hao watapatiwa mafunzo ambayo yasaidia kuimarisha utendaji wao lakini pia kwenda kuwawezesha Maafisa Elimu Kata na Walimu Wakuu ambao ni watekelezaji wa mradi huo moja kwa moja kwenye maeneo yao.

Akitoa neno la shukrani Mhandisi William Thomas Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi amesema watatekeleza mradi wa BOOST kwa weledi lakini ametoa rai ya kupatiwa gari ili kukabiliana na changamoto ya usafiri na kutoingiliwa na wanasiasa wanapotekeleza majuku yao kwenye ujenzi wa miradi.

Mafunzo hayo ya siku mbili kwa kanda ya Mwanza yanalengo la kuboresha ujenzi unaozingatia viwango kama ramani, ubora, rasilimali fedha na utunzaji wa mazingira ikihusisha washiriki kutoka Mikoa 12 ya Kagera, Kigoma, Tabora, Mara, Simiyu, Mwanza, Shinyanga, Singida, Rukwa, Kigoma, Katavi na Geita

BOOST ni Mradi wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji wa kwa shule za Msingi na Awali Tanzania Bara unaochangia Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo katika Sekta ya Elimu kuanzia mwaka 2021/2022 hadi 202526 ambao ni sehemu pia ya Lipa kulingana na Matokeo (EP4R).

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti