• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANANCHI BUCHOSA WAASWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU

Posted on: August 31st, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bwana Ismail Ali Ussi amewaasa wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025 kuwachagua Wabunge, Madiwani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ametoa wito huo leo Agosti 31, 2025 wakati akiongea na wananchi katika kijiji cha Bukokwa na maeneo ya jirani wakati akikagua utekelezaji wa ujenzi wa maduka 20 yanayojengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo kwa lengo la kupata chanzo cha kudumu cha ukusanyaji mapato.

Bwana Ussi amewasisitiza wananchi hao kuhusu umuhimu wa kujitokeza kupiga kura na kuzingatia taratibu za kisheria siku ya uchaguzi ili kulinda amani ya nchi. 

Kadhalika amewataka vijana kutokutumiwa na wanasiasa wenye malengo ya kujinufaisha binafsi kwa kuanzisha vurugu, na badala yake amewataka kuwa mabalozi wa amani na mshikamano katika kipindi chote cha uchaguzi.

Aidha, amewasihi katika kuamua ni nani wa kumchagua wahakikishe wanachagua viongozi sahihi ambao wana kiu ya kuwaletea maendeleo kupitia atakayewapigiania kuwaletea huduma bora za kijamii kama maji safi na salama, elimu na pembejeo za kilimo.

Kadhalika, amewaalika kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo ili kuleta maana ya Uchaguzi mkuu ukilinganisha na idadi ya wananchi waliojiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura katika zoezi lililoendeshwa na Tume huru ya Uchaguzi.

Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ni Halmashauri ya nane (08) na ya mwisho kwa Mkoa wa Mwanza kukimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 chini ya kaulimbiu isemayo ‘Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti