• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANANCHI WA BUCHOSA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAJENGEA CHUO CHA UFUNDI STADI (VETA)

Posted on: November 10th, 2023

WANANCHI WA BUCHOSA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAJENGEA CHUO CHA UFUNDI STADI (VETA)


*RC Makalla awaagiza TANESCO na RUWASA kupeleka huduma kuharakisha ujenzi huo*


*Halmashauri ya Buchosa kupata Chuo cha Kwanza*


*Mkuu wa Mkoa awataka vijana kujiandaa na fursa za ajira kutokana na ufundi watakaopata chuoni hapo*


Leo Novemba 10, 2023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amevuka milima na mabonde kufika kwenye Kijiji cha Kayenze kilicho pembezoni mwa Mji wa Nyegunge kwenye halmashauri ya Buchosa kukagua ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA).


Akizungumza na wananchi kwenye eneo hilo la ujenzi Mhe. Mkuu wa Mkoa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Bilioni 3 kujenga chuo hicho ambapo amebainisha kuwa kitawajenga kiufundi katika fani mbalimbali vijana wa Buchosa na wilaya ya Sengerema kwa ujumla.

"Halmashauri ya Buchosa mmepata bahati sana, Rais Samia Suluhu Hassan anajenga vyuo kwenye halmashauri 63 kwa wakati mmoja ikiwemo na halmashauri yenu, nawapongeza sana kwa hili maana vijana wetu hapa watapata ujuzi kwenye fani mbalimbali ambapo itawasaidia kupata nafasi kwenye miradi ya ujenzi kama wa barabara" Makalla.

Makalla ametumia wasaa huo kuziagiza TANESCO na RUWASA kuhakikisha wanapeleka huduma za umeme na maji kwenye ujenzi huo ili kurahisisha shughuli zinazoendelea kwa kasi kwenye eneo hilo ambapo ndani ya wiki mbili tangia waanze ujenzi wamekwishafikisha asilimia 18 ya ujenzi.

"Umuhimu wa VETA hii ni mkubwa sana kwa vijana fani nyingi zitatolewa hapa kama umeme, mapishi, useremala, bomba na uashi hivyo itakua ni nafasi ya kijana kuamua asomee nini ili akajishughulishe mtaani kwenye kuinua uchumi wake." Amesisitiza Makalla.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Sengerema Mhe. Dominic Makoye amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa kusimamia utekelezaji wa Ilani na ametoa wito kwa wataalam kuendelea kutoa ushirikiano kwenye kukamilisha mradi huo kwa manufaa ya vijana wa Buchosa.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani wa Kata ya Nyehunge Mhe. Dickens Kulwa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa mradi huo ambao ameutaja kuwa unawasaidia wananchi kupata fedha kutokana na shughuli ndogondogo wanazofanya kwenye mradi huo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti