• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wananchi wa Kisesa-Kayenze Wilayani Magu kunufaika na Miradi ya Barabara

Posted on: June 3rd, 2022


Leo Juni 03, 2022 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel amekagua ujenzi wa barabara ya Kisesa-Kayenze wilayani Magu yenye urefu wa KM 10 inayogharimu Tshs Milioni 134 kiwango cha Changarawe ambapo amemuagiza Mkandarasi kukamilisha kwa wakati na kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuimarisha mitaro ya maji ili iweze kudumu muda mrefu.


Akikagua Mradi wa Vyumba vinane vya madarasa vilivyotekelezwa kwa Tshs. Milioni 160, Mhe.Mhandisi Gabriel kwenye shule ya Sekondari Lugeye ametoa rai kwa wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii na kufanya mazoezi ya viungo ili waweze kufaulu kwenye mitihani yao.


"Kwanza mtangulizeni Mungu, pili epukeni tabia mbaya ya mahusiano shuleni, someni kwa bidii mtafanikiwa huu ni wakati wa kutengeneza maisha yako tena somo la hesabu lipeni kipaumbele." Mkuu wa Mkoa.


Mwanafunzi Melesiana Sylivester wa Kidato cha nne katika shule ya Sekondari Lugeye ajipatia zawadi ya papo hapo zaidi ya Shilingi elfu 60 kutoka kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa baada ya kujibu vizuri swali la somo la Hesabu alipoulizwa njia zinazotumika kukokotoa 'simultaneous equation'.


Vilevile, Mhe Mkuu wa Mkoa amefanya ziara kwenye Mradi wa Maji ya bomba Kahangara wenye thamani ya zaidi ya Milioni 500 huku ukitarajiwa kuwahudumia zaidi ya watu 9600 ambapo amewapongeza RUWASA kwa utekelezaji wa mradi huo ambao utawapunguzia wananchi umbali wa kutembea kutafuta huduma hiyo na upatikanaji wa maji salama utapanda hadi 86% kutoka %34 za hivi sasa kwenye eneo hilo.

Aidha, Mhandisi Gabriel amekagua mradi wa jengo la X-RAY na Ultra Sound wenye thamani ya Milioni 66.2 katika Kituo cha Afya Kahangara na amesisitiza marekebisho kwenye dosari chache zilizobainishwa ili mradi uwe nadhifu na uweze kutoa huduma bora kwa wananchi.


"Naomba mazingira ya shule hii yawe vizuri na rafiki kwa kutolea elimu kwa watoto wetu, hakikisheni kule nje kote kunakua sawa" Amesema Mkuu wa Mkoa wakati wa kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Msingi Bugomba kwa zaidi ya Milioni 89.

Milioni 90 zinazotekeleza ujenzi wa nyumba 3 za watumishi hospitali ya Magu zimemfikisha Mhe. Mkuu wa Mkoa kwenye mradi huo ambapo ameagiza ukamilishwaji wa kujibana ili fedha hizo ziweze kusaidia kuboresha mambo mengine kwenye mradi huo kama kupata makabati au matanki ya maji kwenye nyumba hizo tatu za mfumo wa pamoja.


Mhe.Mhandisi Gabriel amekagua pia mradi wa kampeni ya Lishe, Ziro Malaria na kampeni ya VVU/UKIMWI katika hospitali ya wilaya Magu na ametoa wito kwa wananchi kula vyakula vyenye lishe bora katika kujikinga na maradhi mbalimbali na kuzingatia usharudi wa kitaalamu kujikinga na maambukizi ya Malaria na VVU/UKIMWI.

Aidha, amebainisha kuwa ni lazima Halmashauri ishiriki kutokomeza Matatizo ya utapiamlo kwa watoto kwa kushirikiana na wataalamu wa masuala ya lishe kwa kupanga na kutoa fedha kwenye sekta hiyo muhimu kwa amendeleo ya ustawi endelevu.

Mradi wa Anuani za makazi umebainisha kuwa Nguzo za Majina ya mitaa na Barabara wilayani humo umefikia zaidi ya asilimia 50 na ndipo Mhe.Mkuu wa Mkoa akatoa wito kwa watendaji wa zoezi hilo kuwa wabunifu ili kutumia Rasilimali chache zilizopo kukamilisha zoezi hilo nyeti.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti