• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANANCHI WA NGUDAMA - MISUNGWI WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUJENGEWA BARABARA

Posted on: September 13th, 2024

WANANCHI WA NGUDAMA - MISUNGWI WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUJENGEWA BARABARA


Wananchi wa kata ya Bulemeji na Idetemia Wilayani Misungwi wameishukuru Serikali inayongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 8 kwa kiwango cha changarawe pamoja na daraja vinavyogharimu zaidi ya Milioni 427.

Shukrani hizo za wananchi zimetolewa leo ijumaa septemba 13, 2024 kwenye ziara ya Mhe. Mkuu wa Mkoa wakati akikagua mradi wa daraja linalounganisha vijiji vya Ngudama na Kaluluma linalojengwa kwa zaidi ya milioni 122 katika kijiji cha Ngudama.

Akiongea kwa niaba ya wananchi Diwani wa Kata ya Bulemeji Mhe. Rahma Emanuel amesema mradi huo umewapa heshima wananchi ambao awali walilazimika kulipa zaidi ya Shilingi elfu 7 kwa usafiri wa pikipiki kutokana na ubovu wa barabara lakini kwa sasa wanatumia Tshs. 2000 pekee.

Katika wakati mwingine Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa 6, Matundu 10 ya vyoo na Ofisi ya Walimu kwenye Shule mpya ya Sekondari Mwasonge inayojengwa kwa zaidi ya milioni 121 kutoka serikali kuu (Sequip) na akaagiza ukamilishaji unaozingatia ubora.

Aidha, katika kituo cha mabasi cha Misungwi Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua mradi wa ujenzi wa vyumba 20 vya maduka vilivyojengwa kwa zaidi ya milioni 79 kutoka fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo umebuniwa kwa ajili ya kusaidia kuongeza mapato ya Halmashauri kwa kupangisha na kwamba zaidi ya Milioni 8.5 zinatarajiwa kukusanywa kwa mwaka.


Kabla ya kuhitimisha ziara yake kwa kuwataka wananchi kutunza amani na kujiandaa kushiriki kilele cha Mwenge wa Uhuru 2024 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mhe. Mtanda amekagua jengo la Mionzi kwenye kituo cha Afya Misasi lenye thamani ya Milioni 68 na amewataka wananchi kutunza miundombinu hiyo ambayo pamoja na vifaa tiba vinagharimu milioni 302.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti