• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wananchi wanao ishi jirani na mradi wa Ihelele Wilayani Misungwi watakiwa kutunza mazingira

Posted on: March 10th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima amewataka wananchi wanaozunguka kulinda chanzo cha Maji Ziwa Victoria Ihelele  kwenye Kijiji cha Nyangomang'ho kata ya Ilujamate kutunza chanzo hicho kinachohudimia wananchi takribani 1,250,000 (2021) kwenye Mikoa mitano.

Akikagua Mradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama-Shinyanga (KASHWASA) unaozalisha takribani mita za Ujazo 63,000 kwa siku, leo Machi 02, 2023 Mhe. Malima amesema jamii ina wajibu wa kuutunza mradi huo kwa dhati na kujiepusha na shughuli za kiuchumi zinazochafua Maji na kuharibu mazingira.


"Huu mradi ni wa kitaifa, watanzania wengi wanapata maji kutoka hapa Ihelele, siku za nyuma nilipata kusikia kuwa Maji yanayotumika Tabora yanatoka kwenye Chanzo cha Ihelele na leo nimefurahi kufika hapa na kuuona mradi huu kwa macho yangu mwenyewe." Malima.

Mkurugenzi wa Bonde la Ziwa Victoria Mhandisi Renatus Shinhu amesema taasisi hiyo imepanda Zaidi ya Miche ya Miti elfu 8 na kwamba pamoja na afua zingine wametumia Zaidi ya Milioni 250 kuhifadhi mazingira ya bonde hilo na imesadia kuongeza ubora wa Maji na kurejesha na uoto wa asili ambao ulianza kutoweka.

"Chanzo hicho kinakabiliwa na uharibifu wa Mazingira ukiwemo ufugaji wa kilimo ndani ya hifadhi, ukataji wa miti kwa ajili ya kuni, uchomaji wamkaa na matofali na uvuvi wa samaki usio endelevu na kwamba hayo yanasababisha uchafuzi wa chanzo na kupelekea kuongezeka kwa gharama za kutibu Maji." Mhandisi Shinhu.

Aidha, Mkurugenzi huyo amebainisha kuwa ziwa Victoria lina ukubwa wa Kilomita za Mraba 68,800 na kwa upande wa Tanzania ni 35,700 na kwamba ziwa hilo lima Maji kiasi chan Mita za Ujazo Bilioni 2,700 na ka upande wa Tanzania ni Bilioni 1,400.

Naye, Mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama-Shinyanga (KASHWASA) Mhandisi Patrick Nzamba amefafanua kuwa chanzo hicho kina uwezo wa kuzalisha Lita Milioni 80 hadi 120 kwa siku na kwamba kwa sasa wanazalisha Lita Milioni 63 na kwamba gharama kubwa za uzalishaji na wateja kutolipa kwa wakati Ankara zao zinaathiri uendeshaji wa mradi.

Chanzo cha Maji ziwa Victoria Ihelele kinatumiwa na Mamlaka ya KASHWASA kusambaza Maji katika Mamlaka zilizopo katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Tabora, Singida na Simiyu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti