• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANANCHI WANAOTAKIWA KUFIDIWA KUPISHA UWANJA WA NDEGE MWANZA WATAKIWA KUWA NA SUBIRA

Posted on: February 21st, 2025

WANANCHI WANAOTAKIWA KUFIDIWA KUPISHA UWANJA WA NDEGE MWANZA WATAKIWA KUWA NA SUBIRA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewasihi Wananchi wa mitaa mitano iliyoko katika Kata ya Shibula Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza wanaokabiliwa na mgogoro wa mpaka wa uwanja wa ndege kuwa watulivu wakati serikali ikiendelea kutafuta suluhu.

Mhe. Mtanda ameyasema hayo leo Februari 21, 2025 alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Mitaa hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mtaa wa Nyamilolelwa na kuwataka kuendelea kuwa wastahimilivu wakati Serikali ikiendelea na uchakataji wa upatikanaji wa suluhu.

Mkuu wa Mkoa amefanya mkutano huo ikiwa ni mara baada ya Mbunge wa Jimbo la Ilemela kuuliza swali bungeni la ni lini serikali itawalipa fidia wakazi wa mitaa mitano ya kata ya Shibula ambapo majibu ya Waziri wa ardhi alisema kuwa wananchi hao wapewe viwanja mbadala kauli iliyozua utata na mkanganyiko baina ya wahanga hao.

Akuzungumza na Wanachi hao, Mkuu wa Mkoa amesema Serikali inaendelea na mchakato wa majadiliano ili waje na uamuzi sahihi ambapo kwa siku ya leo yeye pamoja na Kamati ya Usalama Mkoa wameamua kuja uwandani kwa lengo la kujionea eneo la mgogoro wawe na uelewa wa pamoja ili waweze kuishauri Wizara na Serikali kuhusu utatuzi wa mgogoro huo.

Mimi kama Mkuu nimeona ni lazima niende na kamati yangu ya usalama kutembelea uwandani, wote hapa tulikuwa hatujafika eneo la mgogoro na ninatambua tayari kuna tathmini kadhaa zimeshafanyika ikiwemo ile ya kwanza ya shilingi bilioni 19, tathmini ya pili ya bilioni 26 nimekuja kuwaomba endeleeni kuwa wastahimilivu. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kama Serikali ya Mkoa haijapokea taarifa kamili ya maandishi  kuhusu uamuzi wa kauli hiyo iliyotolewa na Waziri wa ardhi hivyo wataendelea kujadiliana na kusubiri tamko rasmi la kimaandishi.

“Tunaendelea kutafuta ufumbuzi wa jambo hili na kwa kuwa tayari tumeshakusanya maoni yenu, na maoni yenu yote matano mliyotupatia,  tupeni muda kama serikali ili tuweze kushauriana vizuri na tuje na muafaka”.

Mgogoro huo wa mipaka ya uwanja wa ndege Mkoa wa Mwanza umedumu kwa takribani miaka 8 sasa ambapo Mkuu wa Mkoa amesema yuko tayari kuhakikisha Serikali inaumaliza mgogoro huo kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni sikivu na watafikia maamuzi ambayo ni sahihi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti