• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANAWAKE MWANZA WAJA NA SACCOS MOJA KUWAUNGANISHA MAKUNDI YOTE

Posted on: November 6th, 2024

WANAWAKE MWANZA WAJA NA SACCOS MOJA KUWAUNGANISHA MAKUNDI YOTE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewapongeza wanawake mkoani humo kwa kuazisha SACCOS itakayowaunganisha kwenye sekta ndogo ya fedha na kuhakikisha wanakua kitu kimoja kwa kuwaunganisha makundi yote ndani ya mkoa huo.

Mhe. Mtanda ametoa pongezi hizo leo Novemba 06, 2024 katika hafla ya ufunguzi wa semina ya uhamasishaji wa kuanzisha SACCOS ya wanawake Mkoani humo iliyofanyika katika ukumbi wa Nyanza Coperative Union.

Aidha, amewataka wanawake hao kuitumia vizuri Ofisi ya Mrajisi Msaidizi na CRDB foundation kupitia programu ya IMBEJIMU kupata elimu ya fedha, umuhimu wa kuhifadhi sehemu salama, elimu ya biashara na ikasaidie kuwapa elimu akina mama wengine ili waweze kukuza mitaji.

"Sekta ya fedha inajumuisha taasisi zote zinazojihusisha na huduma ya fedha zikiwemo microfinance ambapo kwa sehemu kubwa ni SACCOS, hii imedhihirisha ukweli kwamba sekta hii inayogusa vikundi vya wananchi wa hali ya kati na chini imekua na mchango mkubwa katika kuimarisha uchumi wa nchi." Mtanda.

Akisisitiza umuhimu wa SACCOS, Mhe. Mtanda amesema mwaka 2024 Mwanza imesajili SACCOS hai 41 kwenye mfumo wa kielekitroniki na kupatiwa leseni za biashara  zenye wanachama 14, 000 wenye hisa na wana amana za bilioni 27.7 na kwamba mikopo iliyotolewa kwa wanachama hao ni Bilioni 2.4.

Hilda Boniface, Mrajisi Msaidizi wa vyama vya Ushirika Mkoa wa Mwanza amesema lengo la kuanzisha chama hicho ni kuunganisha vyama mbalimbali ndani ya Mkoa wa Mwanza na kuwa na chama kikubwa na imara kama vyama vya mazao zaidi ya 200, vyama 24 vya wavuvi, akiba na mikopo 41.

Vilevile, amesema kupitia umoja huo wanawake watahamasisha uzalishaji kwenye zao la pamba ambalo kwa sasa limekua likisuasua, kukomesha kabisa wizi wa samaki kwenye vizimba vya kisasa vya wavuvi pamoja na kukomesha tabia ya kutorejesha mikopo kwa wanachama kwenye vyama vya akiba na mikopo.

Aidha, amefafanua kuwa kupitia umoja huo itakua fursa sasa kwa makundi mbalimbali ya kitaaluma kujiunga kwa kujisajili kama fungamani za pamoja na kuhakikisha kunakua na chombo kimoja imara kiuchumi ndani ya mkoa wa Mwanza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti