• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WARATIBU WA TASAF WAAGIZWA KUSIMAMIA MIRADI KWA UKAMILIFU NA UTIMILIFU

Posted on: August 12th, 2025

Waratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Mkoa wa Mwanza wametakiwa kusimamia miradi ya maendeleo kwa umakini, ubora na viwango ili iwe yenye tija kwa wananchi na idumu kwa muda mrefu.

Rai hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bi. Salome Mwakigomba katika kikao cha Wataalam cha Tathmini ya utekelezaji wa kipindi cha pili cha Mpango wa TASAF Mkoa wa Mwanza.


Bi. Mwakigomba amewataka Waratibu hao kusimamia miradi hiyo iwe endelevu na ikamilike kwa wakati, ambapo amesema wao nia yao ni kuiunga mkono Serikali kwa kuibua na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hivyo pia ni lazima ijengwe kwa ufanisi ili idumu.


“Ni mtarajio na matamanio yetu kwamba miradi yetu hii ya TASAF itekelezwe kwa ubora, kwa mfano mimi nimesoma shule ya Jitegemee imedumu kwa muda mrefu bila kuharibika hivyo natamani hata miradi yetu idumu pia kwa kipindi kirefu”.


Kazi ya TASAF ni ibada unamsaidia mtu kula na kujikimu, hukumu ya mwisho inasema nilikuwa na njaa ukanipa chakula, kwa sasa Mtu anaweza kujitafutia na akapata kitu hiyo ni ibada. Tusichukulie kazi kama kazi tuchukulie matokeo ya kazi na wangapi watanufauka katika ubora ule ule. Amesema Bi. Mwakigomba.


Aidha ametoa muda wa mwezi mmoja hadi kufikia septemba 10, miradi yote ya TASAF katika Mkoa wa Mwanza iwe imekamilika na kukabidhiwa kwa kuwa hakuna kikwazo chochote cha rasilimali hivyo hakutakuwa na sababu yoyote ya kushindwa kufanya hivyo.


Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa, Mhandisi Chagu Ng’oma Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu ametoa wito kwa Waratibu hao wa TASAF kushirikiana kwa ukamilifu na Wahandisi wa Wilaya katika miradi ya ujenzi ili kuwepo na ubora, viwango katika utekelezaji wa miradi.


Amesisitiza kuwa uwepo wa wazo na ushauri kutoka kwa Wahandisi kwa pamoja na waratibu mashauriano hayo ni bora na yanaweza kuleta mchango chanya katika utekelezaji ili kupatikana kwa miradi bora.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti