• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WATUMISHI RS MWANZA WAFANYA ZIARA UTALII WA NDANI HIFADHI YA SERENGETI

Posted on: February 14th, 2025

WATUMISHI RS MWANZA WAFANYA ZIARA UTALII WA NDANI HIFADHI YA SERENGETI


Watumishi zaidi ya 30 kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza leo Februari 14, 2025 wamefanya ziara ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SNP) kwa ajili ya kushuhudia vivutio mbalimbali vya utalii.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, kiongozi wa msafara huo Mkuu wa Seksheni ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi ndugu Kusirie Swai amesema ziara hiyo imelenga kutoa hamasa ya utalii wa ndani kwa watumishi wa Mkoa wa Mwanza.

Amesema sambamba na hilo ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutangaza na kukuza sekta ya utalii nchini kwa kutembelea vivutio mbalimbali.

Ndugu Swai amesisitiza kuwa ziara hiyo imewapa fursa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kujionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwemo wanyama wakubwa kama vile Simba, Tembo, Faru, Nyati na Chui wakiwa katika mazingira ya asili yaliyohifadhiwa vizuri.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Jesca Lebba akiwa ni miongoni mwa watumishi walioshiriki ziara hiyo ameushukuru uongozi wa Mkoa chini ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Said Mtanda na Katibu Tawala Mkoa Bw. Balandya Elikana kwa juhudi kubwa wanazofanya kwa watumishi hao ambapo wameitaja ziara hiyo kuwa itakwenda kuongeza tija na hamasa katika utendaji wa majukumu yao kutokana na mapumziko mujarabu.

"Ziara hii ya kitalii itasaidia kuhamasisha watumishi wengi zaidi kutembelea hifadhi wakiwa na familia zao wakati mwingine kwa kuwa wameshaona umuhimu wa kufanya hivyo kiafya kwani inapunguza hata msongo wa mawazo”. Amesema ndugu Paulo Zahoro, Afisa Habari wa Mkoa.

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni mbuga kubwa ya kitaifa ambayo ina urefu wa zaidi ya kilomita za mraba 14,763 Ipo mashariki mwa Mkoa wa Mara na kaskazini mashariki mwa Mkoa wa Simiyu na ina zaidi ya hekta milioni 1.5 Hifadhi hiyo ilianzishwa mnamo 1940.


Aidha Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni urithi wa Dunia iliyojaa wanyamapori zaidi ya wanyama milioni 2, simba 4000, chui 1000, duma 550 na aina 500 za ndege wanaishi katika eneo linalokaribia kilomita za mraba 15,000 kwa ukubwa.


Watumishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wapo kwenye mpango thabiti wa kupumzika kwa kufanya utalii katika hifadhi mbalimbali nchini pamoja ni kuangalia utekelezaji wa miradi ya Kimkakati ambapo kesho februari 14, 2025 wanatarajia kutembelea Mamlaka ya Ngorongoro.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti