• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Watumishi wa kujitolea wakumbushwa kufanya kazi kwa bidii na weledi

Posted on: August 15th, 2022


Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza Joachim Otaru, ametoa rai kwa watumishi wa Afya wanaojitolea kujituma ili kusaidia juhudi za Serikali za kuboresha huduma za afya kwenye maeneo watakayonufaika na mradi wa kuwalipa nusu ya mshahara wa ajira rasmi.

Ametoa wito huo mapema leo Agosti 15 2022 wakati akimwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza kwenye hafla ya Uzinduzi wa mpango wa kujitolea kwa watumishi wa huduma za afya unaoratibiwa na Taasisi ya Mkapa kwa kushirikiana na Serikali utakaowanufaisha watumishi 152 Mwanza na Simiyu.

Vilevile, ndugu Otaru amezipongeza Wizara za TAMISEMl na Afya kwa kupandisha hadhi vituo vya kutolea huduma kutoka Zahanati kuwa Vituo vya Afya au Hospitali za Wilaya na wadau mbalimbali wanaoshiriki juhudi za Serikali za kuboresha huduma za Afya huku akibainisha kuwa mradi huo utasaidia kukuza ujuzi na uzoefu kwa wataalamu hao wakati wakisubiri ajira rasmi.

"Nawapongeza taasisi hii kwa kuamua kutusaidia kupunguza tatizo la upungufu wa wahudumu kwenye sekta ya afya, pia natoa wito kwa mchakato wa kuwapata watoa huduma hizi uzingatie miongozo na taratibu za kiutumishi kwa kupata sifa stahiki nasi tupo tayari kushirikiana nao." Amesema, Katibu Tawala Msaidizi, Utumishi na Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  Mwanza, Daniel Machunda.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Deogratius Kayombo ameishukuru taasisi hiyo kwa kuona tatizo na kuchukua hatua kushirikiana na Serikali kwenye kutatua ama kupunguza Upungufu wa watoa huduma za afya ambao kwa kuanzia mradi huo unatekelezwa kwenye mikoa ya Mwanza, Simiyu, Lindi na Mtwara.

Dkt. Ellen Senkoro kutoka Mfuko wa Benjamin Mkapa amesema kutokana na tatizo la upungufu wa 50% ya watumishi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, taasisi hiyo iliandaa muongozo wa kujitolea kwa Watumishi wa Idara ya Afya ambao ulizinduliwa Septemba 2021 na Waziri wa Afya ukilenga.

Aidha, Dkt Senkoro amefafanua kuwa mpango huo utasaidia kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, Kupambana na maambukizi ya UKIMWI/VVU, huduma za Chanjo ya Uviko 19 na zingin na kwamba taasisi hiyo imeshaajiri watumishi 4159 na Asilimia 50 wamehuishwa kwenye ajira rasmi za Serikali kadiri vibali vya ajira ya afya vinapotolewa na serikali.

Warsha hiyo imewashirikisha Waganga wakuu wa Halmashauri, Maafisa Utumishi wa Mikoa, Makatibu wa Afya, Mashirika yasiyo ya serikali, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wizara ya Afya na wizara ya TAMISEMl.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti