• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Watumishi wa Umma watakiwa kufanya kazi kwa bidii

Posted on: October 3rd, 2019

Watumishi wa umma wametakiwa kufanya kazi kwa utii, kuzingatia sheria,kanuni na miongonzo ya utumishi katika utoaji huduma bora kwa wananchi pamoja na kutumia taaluma zao kuleta mabadiliko chanya.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Dkt.Mary Mwanjelwa wakati akizungumza kwenye mkutano na watendaji wa taasisi za umma Mkoani Mwanza alisema,wananchi wote wanahitaji huduma mbalimbali kutoka Serikalini ambao wanatoa huduma hizo ni watumishi wa umma,hivyo katika kutekeleza hilo wanapaswa kufanya kazi kwa utii na kuzingatia sheria na siyo kwa mazoea.


"Mtumishi wa umma anapaswa kufanya kazi mahali popote kwa utii na wajibu wake ni kutoa huduma bora kwa wananchi pamoja na kuwa mbunifu,mvumilivu na mzalendo licha ya kuwa changamoto zipo, anatakiwa kutumia utaalamu na weledi wake kuleta mabadiliko chanya mfano eneo ambalo mapato yake ni kidogo kupitia yeye yaongezeke palipo na utovu wa nidhamu na maadili yawepo," alisema Dkt.Mwanjelwa.


Pia alisema,kitendo cha mamlaka za nidhamu kutozingatia sheria, kanuni na taratibu wakati wa kushughulikia masuala ya nidhamu kinaisababishia Serikali hasara pale inapolazimika kuwalipa watumishi mishahara ambayo hawakifanyia kazi ikiwa pamoja na kuanzishwa upya kwa mashauri hayo na watumishi kurejeshwa kazini.


"Kutokana na kitendo hicho nawaagiza watendaji wakuu wa taasisi zote za umma kuhakikusha kwamba mashauri ya nidhamu yanaendeshwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma,hivyo wale ambao watakiuka tume ya utumishi wa umma izijulishe mamlaka zao za nidhamu stahiki zichukuliwe dhidi yao mara moja," alisema.


Aidha alitumia fursa hiyo,kuwaagiza kila mwajiri kuhakikisha watumishi wake wanapata elimu kuhusu dhana nzima ya OPRAS ili waweze kuielewa na kutekeleza kikamilifu,wanajaza kikamilifu na kufanya tathmini ya utendaji kazi wao kwa ajili ya kuhakikisha malengo yaliyowekwa na taasisi yanafanikiwa.


"Suala la ujazaji OPRAS ni takwa la kisheria kama inavyobainishwa na kifungu cha 6 cha sheria ya utumishi wa umma sura ya 298,hata hivyo takwimu zinaonesha kuwa suala hilo bado halipewi umuhimu unaostahili,taarifa za kaguzi mbalimbali zinazofanywa na tume kuhusu usimamizi na uendeshaji wa masuala ya rasilimali watu zinaonesha kuwa OPRAS bado ni changamoto kubwa kiutekelezaji hivyo waajiri wanapaswa kulisimamia jambo hilo," alisema.


Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Christopher Kadio alisema, manufaa ya mkutano huo ni kufumbuliwa macho kwa kuwajengea uelewa mzuri wa sheria ya utumishi wa umma na kugundua miongoni mwao wapo watu ambao watawatumia katika kuboresha sekta hiyo pamoja na kupata fursa ya kutambua matatizo yao huku akiwahimiza watendaji na watumishi kujitoa katika kuhudumia wananchi kwa maendeleo ya taifa.


Naye Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma Balozi Mstaafu John Haule alitoa wito kwa watendaji wa taasisi za umma kuwapa fursa na kuwatumi maofisa utumishi na wanasheria kwani wanajua tafsiri za sheria hiyo ya utumishi huku mamlaka zitakazokuwa tayari kugharamia watumishi wake timu ya tume hiyo itakuja kuwaelimisha namna ya kutekeleza sheria,kanuni na taratibu za utumishi wa umma.


Aidha Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Cornel Magembe alisema,tume ya utumishi wa umma ifungue milango wazi watu wakasome wasilazimishwe kusomea kitu alichonacho mwanzo mfano walimu wapewe fursa ya kusomea vitu vingine ili wasaifie jamii katika nyanja nyingine huku Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Dkt.Severine Laika aliomba mafunzo ya OPRAS yaongezwe kwani ni nzuri.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti