• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Waziri Mkuu Majaliwa asisitiza nidhamu ya matumizi ya fedha za miradi

Posted on: October 17th, 2022

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) ametaka kuwepo na nidhamu nzuri ya matumizi ya fedha za Miradi ya Maendeleo akitoa mfano wa kuigwa Wilaya ya Ukerewe Kisiwa cha Irugwa.

Akizungumza leo Kisiwani Irugwa wakati wa ukaguzi wa vyumba vya madarasa 6 shule ya Sekondari Irugwa vilivyogharimu Tshs milioni 120 na kutumika Tshs milioni 119, Mhe. Majaliwa amesema kwa jiographia ya Kisiwa hicho na nidhamu ya matumizi ya fedha hizo wahusika wote wanastahili pongezi.

"Leo nawapa zawadi ya Tshs Milioni moja mkagawane kwa nidhamu mliyoonesha maana natambua changamoto ya kuleta Vifaa hapa vya ujenzi lakini bado mmetumia fedha vizuri na chenji kubaki, Viongozi wengine nataka wapate ujumbe huu." Amesisitiza  Waziri Mkuu.

Mhe. Majaliwa amebainisha kuwa bado kuna changamoto sana ya matumizi ya fedha za Serikali zinazolengwa kuwaletea Maendeleo wananchi na kusisitiza hatakuwa na huruma Kwa Viongozi wenye tabia hizo.

Aidha, Waziri Mkuu ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kisiwani Irugwa kilichogharimu Tshs milioni 500 na kuahidi kuletwa kiasi cha Tshs milioni 270 kwa ajili ya kukiboresha Kituo hicho kiwe na matibabu yote ya msingi likiwemo jengo la Mama na Mtoto.

Akijibu hoja ya Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe Denis Mwila kuhusiana na ubabaishaji wa Mkandarasi wa barabara za ndani mjini Nansio kampuni ya Inter Country inayomilikiwa na Mazoa Nyakilagani, Mhe. Majaliwa ameagiza Mkandarasi huyo kufika Ofisini kwake Dodoma wiki hii ili kujibu tuhuma za kuzembea kukamilisha Mradi huo.

Kuhusu kero ya usafiri wa Mitumbwi Kisiwani humo Mhe. Majaliwa amewaahidi Wakazi hao kulibeba suala hilo na kwenda kulifanyia kazi ili wapate kivuko cha uhakika.

Awali akimkaribisha Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema Mkoa huo umeendelea kunufaika na Miradi mbalimbali ya Maendeleo kuanzia Sekta ya Afya, Elimu na Miundombinu.

"Mhe. Waziri Mkuu Kisiwa cha Irugwa kipo mbali sana kutoka mjini Nansio na wakazi wa huku huduma za haraka kwao wanazipata Mkoani Mara ambako ni karibu hivyo kuwaletea huduma zote za msingi hapa kutawapunguzia usumbufu," amesema Mkuu wa Mkoa.

Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa anaendelea na ziara yake mjini Mwanza kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Stendi ya m

Mabasi ya Nyegezi na ujenzi wa Meli mpya Mv Mwanza Hapa Kazi tu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti