• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa kufanya ziara ya siku nne Mwanza

Posted on: October 13th, 2022


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) anatarajiwa kuwasili Mkoani Mwanza Jumamosi ya Oktoba 15, 2022 Majira ya saa 10 jioni kwa ziara ya kikazi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkoa  mapema leo alhamisi Oktoba 13, 2022.

Mhe. Malima ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi wa Mwanza na Mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kandokando ya barabara na kwenye Miradi atakayoitembelea kumlaki na kumpokea Kiongozi huyo ambaye atakuwepo mkoani humo kwa ziara ya siku nne.

"Nawaomba wakaazi wa Mwanza tuoneshe uzalendo wa dhati, sote tuungane kumpokea Mgeni wetu na tumwoneshe mapenzi ya dhati huku tukiishukuru Serikali kwa kutuletea Maendeleo kama tunavyoona Miradi mbalimbali inaendelea kutekelezwa kwenye maeneo yetu." Mkuu wa Mkoa.

Akizungumzia ratiba ya ziara amesema ,siku ya jumapili ya Oktoba 16, 2022 kuanzia Majira ya saa 2 asubihi Mhe. Majaliwa atakagua Maendeleo ya Ujenzi wa Daraja la Magufuli Kigongo-Busisi pamoja na kusalimia wananchi wa Busisi kabla ya kuelekea wilayani Kwimba ambako atakagua Maendeleo ya Ujenzi wa Mradi wa Reli ya kisasa (SGR).

Malima amefafanua kuwa katika siku hiyohiyo, kuanzia Majira ya saa 7 mchana Mhe. Waziri Mkuu atazindua Jengo la Huduma ya Macho kwenye Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando pamoja na kuzungumza na  wananchi kwenye uwanja wa Mahafali hospitalini hapo.

"Siku ya tatu ya ziara ya Mhe. Waziri Mkuu itaanzia Wilayani Ukerewe kwenye visiwa vya Irugwa majira ya saa 3 asubuhi ambako atakagua ujenzi wa Kituo cha Afya na Maendeleo ya Shule ya Sekondari ya Irugwa kabla ya kuelekea kisiwani Gana ambako akiwa huko atakagua maendeleo ya Ujenzi wa Zahanati pamoja na kusalimia wananchi." Amesema Mhe. Malima.

Ameongeza kuwa mara baada ya shughuli za visiwani Mhe. Waziri Mkuu atarejea Mjini Mwanza ambako anatarajiwa kukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Nyegezi kuanzia Majira ya saa 9 alasiri na baadae atawasili bandari ya Mwanza Kusini kwa ajili ya kukagua maendeleo ya Ujenzi wa Meli ya MV Mwanza 'Hapa Kazi Tu'.

Awali amefafanua kuwa Mkandarasi anayejenga Barabara za Mjini Ukerewe kwa kiwango cha Lami Nyepesi kuikamilisha ifikapo Oktoba 15, 2022 kama alivyoagiza alipofanya ziara wilayani humo mwezi uliopita na ametoa wito kwa watumiaji wa Vyombo vya Moto kuziangatia Sheria za Usalama Barabarani ili kuwalinda watumiaji na kujiepusha na ajali.  

Vilevile, Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishna Mwandamizi Msaidizi Ramadhani Ng'anzi amesema jeshi hilo pamoja na mambo mengine litahakikisha katika barabara zote zinazoingia Mkoa wa Mwanza hakutakua na Chombo cha Moto kitakachoharibika na kubaki bila kushughulikiwa kwani tabia hiyo imekua ikisababisha ajali na watembea kwa miguu watapewa uangalizi maalumu ili kuwalinda na ajali za Barabarani.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti