• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ZAIDI YA BILIONI 2 KUNUFAISHA WANANCHI UJENZI WA MINARA YA MAWASILIANO MWANZA

Posted on: July 18th, 2024

ZAIDI YA BILIONI 2 KUNUFAISHA WANANCHI UJENZI WA MINARA YA MAWASILIANO MWANZA


Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye (MB) amesema Serikali inatekeleza mradi wa ujenzi wa minara 758 unaogharimu zaidi ya Bilioni 200 utakaonufaisha wananchi Milioni 23.6 kupata huduma bora za mawasiliano ya intaneti, data na simu.

Mhe. Nape amebainisha hayo leo Julai 18, 2024 Wilayani Sengerema alipokua ziarani kukagua mnara wa mawasiliano katika Kisiwa cha Lyakanyasi huku akibainisha kuwa wilaya hiyo itanufaika kwa kujengewa minara 2 kati ya 17 inayojengwa Mwanza.

"Minara hii inajengwa na makampuni ya simu tena inagharimu fedha nyingi sana zaidi ya Milioni 350 kwa mnara mmoja tena kwenye maeneo ambayo hayana mvuto sana kibiashara na kwakweli makampuni mengine yasingeweza kwenda kuwekeza hivyo ni lazima ilindwe." Mhe. Nnauye.

Vilevile, amewasihi viongozi wa wilaya kusimamia upatikanaji wa maeneo ya kujenga minara hiyo itakayosaidia kukuza uchumi vijijini na akatoa wito kwa taasisi zinazotoa huduma za umeme na barabara  kufikisha miundombinu hiyo kwa kipaumbele ili kurahisisha utoaji wa huduma bora pamoja usalama.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga zaidi ya Tshs. Bilioni 2.4 kwa ajili ya kujenga minara 17 katika kata 16, vijiji 52 na inatarajiwa kunufaisha zaidi ya wananchi 296, 410 wa wilaya 5 za Magu, Ilemela, Sengerema, Misungwi na Ukerewe.

Akiwasilisha taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) John Dafa amesema hali ya mawasiliano nchini ni ya kuridhisha kwa zaidi ya asilimia 85 (2G, 3G, 4G) na kwa Mwanza huduma zimefika kwa wananchi kwa wastani wa zaidi ya asilimia 95.

Akizungumzia usajili wa laini za simu amesema Mwanza kuna ongezeko la zaidi ya asilimia 42 kutoka mwaka 2022 kwani wananchi 4,803,249 (Machi 2024) wamesajiliwa kutumia laini za simu na kwamba kuna zaidi ya vituo vya redio 26 mkoani humo kwa sasa.

Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Bi. Justina Mashiba amesema hakuna mtanzania atakaa bila huduma za mawasiliano na kwamba siku za nyuma minara 50 ilijengwa kupitia ruzuku ya awali UCSAF kwa zaidi ya Bilioni 6.6 huku wananchi 885, 420 wakinufaika mkoani Mwanza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti