• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 3 WAPATA MAJI SAFI NA SALAMA MURUTANGA-UKEREWE

Posted on: July 13th, 2023

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 3 WAPATA MAJI SAFI NA SALAMA MURUTANGA-UKEREWE


Mwenge wa Uhuru umezindua Upanuzi wa Mradi wa Maji Murutanga (Tanki la Maji Kagunguli) wenye thamani ya zaidi ya Milioni 279 kutoka chanzo cha Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Uviko 19 wilayani Ukerewe ambao umewanufaisha zaidi ya wananchi elfu tatu.

Akizungumza baada ya Uzinduzi huo leo Julai 13, 2023, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaib Kaim amewapongeza Mkuu wa Wilaya, RUWASA na Watendaji wa Ukerewe kwa ujumla kwa Usimamizi mzuri ulioleta matokeo ya mradi bora unaoendana na thamani ya fedha zilizotumika.

"Mwenge wa Uhuru 2023 umekagua Mradi huu kwa kina na itoshe tu kusema ubora umezingatiwa na hakika RUWASA mmeonesha nia ya kumuunga mkono Mhe. Rais kwa kumtua mama ndoo kichwani na kuwaletea huduma bora ya Maji wananchi." Ndugu Kaim.

Naye, Mbunge Viti Maalumu (CCM) Mhe. Furaha Matondo amesema uwepo wa huduma hiyo utasaidia kuwaondoa wananchi wa Kijiji hicho dhidi ya magonjwa ya mlipuko na tumbo kutokana na uwepo wa maji Safi kwenye makazi yao.

Mapema asubuhi Mwenge wa Uhuru ulifika kwenye Mradi wa Ufugaji Samaki ambapo kiongozi wa mbio za Mwenge ametoa rai kwa Halmashauri kuwainua vijana kwa kuwakopesha fedha kupitia fungu la asilimia 10 za mapato ya ndani ili wakuje mitaji yao na kuweza kuwapa urahisi wa kununua malighafi kama chakula na vifaranga.

Akiweka Jiwe la Msingi kwenye Ujenzi wa Kituo cha Afya Murukilima mradi unaotarajiwa kukamilika Mwezi Septemba mwaka huu kwa kupata Miundombinu yenye thamani ya zaidi ya Milioni 500, Ndugu Kaim amewapongeza kwa Usimamizi mzuri wa mradi ambao utawanufaisha zaidi ya wananchi elfu 58 kwa kupata huduma za afya karibu.

Akikagua shamba la matunda kwenye kijiji cha Gillu lililopandwa miche 2992 aina ya Machungwa na maembe, Ndugu Kaim ametoa wito kwa Mkuu wa Wilaya kufuatilia kwa karibu shamba hilo ili kuipa tija Milioni 27.7 iliyowekezwa na kwenye Madarasa 7 yaliyozinduliwa kwenye Sekondari ya Ilangala ameagiza urekebishaji wa dosari zilizobainika.

Zikihitimishwa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Ukerewe kwa kukimbizwa kwenye miradi sita yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 1.1, Kikundi cha Vijana Ufundi ni Ajira kilihiyimisha mbio hizo kwa kushauriwa Maafisa husika kuwapa mafunzo vijana na wote wanaowakopesha ili waweze kutumia vizuri mikopo yao.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti