• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

CCM YAIPONGEZA SERIKALI UJENZI WA BARABARA YA LAMI BUHONGWA- IGOMA

Posted on: May 27th, 2024

CCM YAIPONGEZA SERIKALI UJENZI WA BARABARA YA LAMI BUHONGWA- IGOMA.


Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza leo 27, Mei 2024 imekagua mradi wa ujenzi wa Barabara ya Lami yenye urefu wa Kilomita 14 (Buhongwa - Kishiri- Igoma)Jijini Mwanza na kumpongeza Mkuu wa Mkoa kwa Usimamizi wa mradi huo na imemtaka kuendelea kusimamia vema mradi huo.

Akiongoza Kamati hiyo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Mhe. Michael Lushinge amemtaka Mkandarasi Zhongmei Engineering group Ltd anayejenga barabara hiyo kwa zaidi ya Shilingi Bilioni 22.7 kukamilisha ujenzi huo kwa wakati kwa mujibu wa mkataba ili wananchi wa Kata nne zinazopitiwa na mradi wanufaike.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema chini ya usimamizi wake kupitia Idara ya ujenzi Jiji la Mwanza pamoja na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) atahakikisha ujenzi unakwenda kwa kasi ili hadi kufikia Februari 2025 uwe umekalimika na kuwandolea wananchi adha ya usafiri.

Ameahidi kuketi na TARURA, MWAUWASA na TANESCO ili kuhamisha kwa hataka miundombinu na kuweza kuharakisha mradi na kwamba atazungumza na ofisi husika ili wakandarasi wapate fedha kwa wakati na kuweza kutekeleza mradi huo wenye manufaa makubwa kwa wananchi.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Erick Mvati amesema kuwa mradi huo wa kuboresha miundombinu ya barabara utahusisha ujenzi wa barabara pamoja na ujenzi wa Ofisi ya Mshauri kwenye Makao Makuu ya Jiji, uwekaji wa taa 470, Makaravati na Mitaro kwa mkataba wa kuanzia Septemba 2023 na hadi Februari 2025.

Ameongeza kwamba Mkandarasi hadi sasa ameshalipwa Shilingi Bilioni 3 na ameomba kuongezewa Milioni 600 na kwamba changamoto kubwa inayoukabili mradi huo ni gharama za uhamishaji wa miundombinu ya Maji, Simu na Umeme pamoja na nyumba zilizopo kwenye eneo la mradi lakini zinaendelea kupatiwa ufumbuzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.