• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi Yahamasishwa Mwanza

Posted on: May 6th, 2019

Jumla ya wanawake 50,000 hapa nchini kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) hupata maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi na hivyo kusababisha asilimia 37 ya wanawake wanaogundulika na ugonjwa kufariki kila mwaka.


Hayo yamesemwa  jijini hapa na Afisa Mpango  wa Chanjo kutoka Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na watoto  Pricella Kinyunyi alipokuwa akieleza lengo mahususi la serikali kuanzisha chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri kuanzia miaka 9- 14 kwenye mkutano wa wadau wa sekta ya afya kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza.


Alisema wagonjwa wengi wa saratani ya mlango wa kizazi hawapati mapema huduma za ugunduzi na matibabu sahihi kwa wakati hali inayosababisha vifo.


“Takwimu kutoka hosipitali ya ocean Road inaonyesha  kwamba, saratani ya mlango wa Kizazi inachangia kwa asimilia 36 ya saratani zote na asilimia 70 ya wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi wanajitokeza katika hatua ambayo tayari saratani imesha sambaa maeneo mengine mwilini,” alisema.  


Aliongeza kuwa chanjo hiyo ya saratani ya mlango wa kizazi ni salama na imethibitishwa na Shirika la Afya Duniani na kwamba majaribio ya matumizi ya chanzo kwa mara ya kwanza yalianzia mkoani Kilimanjaro mwaka 2014 na haikuwa na madhara ya kiafya.


“Matokeo ya chanjo hiyo yalikuwa ni mazuri mkoa ulifikia asilimia 90 ya uchanjaji, lengo hasa lilikuwa ni kupata uzoefu wa kujifunza kwa vitendo kabla ya kwenda nchi nzima,” aliongeza.


Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela katika kuhakikisha ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi unatokomezwa, amewataka wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji na wenyeviti wa halmashauri kuhakikisha wanahamasisha vijana wengi kwenye maeneo yao ili waweze kupata chanjo hiyo.


“ Hatuwezi tu kuruhusu watu kupata huduma za tiba peke yake, lazima tuhakikishe program za chanjo katika mkoa wetu zinaimarishwa,” alisema.


Kwa mujibu wa taarifa za serikali, mkoa wa Mwanza umetekeleza zoezi la chanjo ya kuzuia  saratani ya mlango wa kizazi ambayo ilizinduliwa rasmi April 23 mwaka jana, na kuandikisha jumla ya mabinti 31,291 wenye umri chini ya miaka 14, ambapo uliweza kuchanja jumla ya mabinti 24,628 ikiwa ni sawa na asilimia 79 ya ufanisi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.