• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

JIJI LA MWANZA LAJIELEKEZA KWENYE MATUMIZI BORA YA ARDHI WAJENGA MADARASA MFUMO WA GHOROFA

Posted on: July 15th, 2023

JIJI LA MWANZA LAJIELEKEZA KWENYE MATUMIZI BORA YA ARDHI WAJENGA MADARASA MFUMO WA GHOROFA


Halmashauri ya Jiji la Mwanza yakamalisha Ujenzi wa Madarasa 12 kati ya 16 kwa mfumo wa ghorofa kwenye Shule ya Sekondari ya Mirongo kwa gharama za zaidi ya Sh Milioni 513.5 kutoka vyanzo vya Mpango wa Ustawi wa Taifa na Kuthibiti Uviko 19, mapato ya ndani ya Halmashauri na Serikali kuu.

Hayo yamebainishwa leo julai 15, 2023 wakati Mwenge wa Uhuru ulipofika kuzindua madarasa 12 yaliyokamilika kwa awamu ya kwanza yakiwa na samani ambayo yatasaidia   kuondoa msongamano wa wanafunzi darasani kwani yana uwezo wa kuchukua wanafunzi 600.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa madarasa hayo, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kujenga madarasa kwa mfumo wa ghorofa ambapo yatasaidia kupunguza gharama za ujenzi kutokana na kutumia ardhi ndogo tofauti na endapo wangejenga kwa mfumo wa kawaida.

"Baada ya kukagua nyaraka na ujenzi kwa ujumla, Mwenge wa uhuru umeridhika na ubora na ndani ya siku tano naomba tuyafanyie kazi mapungufu hasa kwenye upande wa viti na meza ili vijana wapate elimu kwenye mazingira bora kabisa kama Mhe. Rais alivyoweka nia hiyo." Ndugu. Kaim.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Nyamaganawa Mhe. Amina Makilagi amefafanua kuwa kwa sasa wanafunzi watakaa kwa uwiano wa 50 kwa darasa tofauti na hali ilivyokua ambapo walilazimika kuketi wanafunzi 100 ndani ya chumba cha darasa jambo ambalo lilipelekea kuwa na mazingira magumu ya ufundishaji na kujifunzia kwa wanafunzi na walimu.

"Miaka 2 nyuma shule za ghorofa jijini Mwanza zilikua tatu tu lakini ndani ya Miaka Miwili ya Rais Samia tumejenga madarasa kwa mfumo wa ghorofa kwenye shule 13, achilia hapa lakini pale bugarika pakikamilika tutakua na madarasa 16, Mkolani, Mandu na Mkuyuni madarasa 24 kwa mfumo huu kwakweli tuwapongeze wote waliosimamia miradi hii." Mhe. Makilagi.

Awali taarifa ya radi huo iliyosomwa kwa mkimbiza Mwenge wa Uhuru ilifafanua kuwa uamuzi kwa Ujenzi wa madarasa hayo kwa mfumo wa ghorofa umetokana na hali ya ongezeko la watu na ufinyu wa ardhi na kwamba kwa ujenzi wa madarasa hayo 16 umeokoa eneo la ardhi la mita za mraba 656 na kwamba fedha zaidi ya milioni 88 zimeokolewa kwenye ardhi.

Mapema asubuhi, Mwenge wa Uhuru umekabidhi mifuko 300 ya saruji kwenye shule ya msingi Samia ambayo yatasaidia katika Ujenzi wa madarasa 10 yaliyoanzishwa na wananchi na baadae ukaangazia kwenye upande wa Sekta ya utawala ambapo umefanyika uzinduzi wa ofisi ya kata ya Mabatini.

Vilevile, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Unguja A kwa kiwango cha lami yenye urefu kwa mita 372 kwa gharama ya milioni 348.1 na kuagiza usimamizi mzuri ili ikamilike kwa ubora na wananchi wakatakiwa kutofanya biashara barabarani na kuhakikisha wanaitunza Miundombinu hiyo.

Kabla ya Mwenge wa Uhuru kufungua mradi wa ujenzi wa wa Miundombinu katika kituo cha afya Bulale na kuagiza urekebishaji wa mifumo ya maji na kutenganisha taa na feni ili mwanga usiwe na mawimbi, mwenge wa uhuru umeweka jiwe la nsingi kwenye jengo la uwekezaji la Family Corner linalojihusisha na makazi (Apartments).

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.