• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maadhimisho ya Miaka 25 ya SAUT,kuja pamoja na kituo cha Ubunifu cha Sayansi na Teknolojia

Posted on: May 11th, 2023

**Maadhimisho ya Miaka 25 ya  SAUT kwenda pamoja na kuanzishwa kituo cha Ubunifu cha Sayansi na Teknolojia*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amesema Maadhimisho ya mwaka huu ya Miaka 25 ya Chuo Kikuu cha Mt.Augustino SAUT yatakwenda pamoja na kuanzishwa Kituo cha Ubunifu cha Sayansi na Teknolojia ambacho kitakuwa mkombozi kwa maendeleo ya vijana hapa nchini.

Akizungumza leo Ofisini kwake katika  Mkutano na Vyombo vya habari pamoja na uongozi wa chuo hicho Kikuu,Mkuu huyo wa Mkoa amesema ndani ya miezi miwili kituo hicho kitakuwa tayari kikijikita kwenye Kilimo,Uvuvi na Ufugaji na kitakuwa chuoni hapo.

Ameongeza kuwa tayari Serikali imeweka mazingira mazuri kwa vijana kwenye sekta ya Kilimo,Uvuvi na Ufugaji,hivyo kuwaongezea ujuzi zaidi kupitia kituo hicho kutaleta mapinduzi chanya katika maendeleo yao hasa kujiajiri wenyewe.

"Serikali ya Mkoa itatafuta maeneo kama pale shamba la mifugo la Mabuki tunaweza kuomba hekari kumi kwa ajili ya matumizi ya vijana kufundishwa Ufugaji bora na wa kisasa wa ng'ombe pia tutazishirikisha baadhi ya Halmashauri kutupatia maeneo rafiki ya Uvuvi na Kilimo,Amesisitiza Mhe. Malima.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha hatua hii itakiingiza Chuo cha SAUT kwenye sura ya kimataifa zaidi kwani mpango kama huu wa ubunifu umefanyika kwenye vyuo vingi maarufu Duniani kama Chuo Kikuu cha  Havard kilichopo Marekani.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa nakuahidi yote uliyozungumza tunakwenda kuyatekeleza hasa hili la kuanzishwa hiki kituo,Wataalamu wa kufanya kazi hii wapo na kila kitu kitakwenda sawa na kukamilika kwa wakati,"Mhe.Balozi.Prof.Costa Mahalu,Makamu Mkuu wa SAUT.

Kilele cha Maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo Kikuu cha Mt.Augustino  kitakuwa ni Novemba 11,2023 huku shughuli mbalimbali za ndani na nje ya Chuo hicho kuelekea Maadhimisho hayo zikianza Mei mwaka huu

SAUT kilianza kuwa Chuo Kikuu mwaka 1998 awali kilijulikana kama Nyegezi Social Training Centre.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.