• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mabadiliko ya Sera ya Kilimo Yafufua matumaini kwa wawekezaji

Posted on: August 6th, 2019


  • Serikali  imepongezwa kwa hatua yake ya kuanza kupitia upya sera ya kilimo  na huku ikiondoa  Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na vikwazo kadhaa kwenye vifaa vya kilimo vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi jambo ambalo litasaidia kuwaondoa wakulima kutoka kilimo cha kujikimu na kwenda cha biashara.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda lake kwenye maonesho ya wakulima Nanenane-Nyamhongolo mkoani Mwanza, Meneja Masoko wa Kampuni ya uuzaji na usambazaji wa  zana za kilimo ya Kirasa Co.Ltd, Omari Msisi alisema  kama wadau wa kilimo wamefurahishwa na hatua hiyo ambayo itatoa fursa kwa wakulima na wafanyabiashara kuwekeza sekta ya kilimo.

Msisi alisema kama wasambazaji wa zana za kilimo wamepokea kwa mikono miwili mpango wa Serikali kuja na uwekezaji mkubwa katika kilimo kitendo ambacho kitasaidia  wakulima kutumia teknolojia katika kufanikisha kilimo cha biashara.

 Msisi alisema  kampuni ya Kirasa  Ltd wamekuwa washirikiana na Serikali katika kufanikisha sekta ya kilimo, hivyo wamelazimika  kupunguza gharama za matrekta yao  aina ya Massey Furguson kwa sababu wameondolewa VAT ambapo  aliwataka wakulima kuchangamkia  fursa hiyo.


“Tumeamua kuleta trakta za kilimo za Massey Furguson ambazo zinatumika kila msimu kwa kubadildihiwa matumizi, wakati wa masika zitatumika kwa kulima mashamba, pia kiangazi zinatumika kusombea mizigo ikiwamo mchanga, tofali au mazao, vile vile zinatumika katika kusaga vyakula na kumwagilia maji kama utalima kiangazi.


“Kutokana na hali ya hewa kubadilika kila msimu, ni vema wakulima wakajikita katika kilimo cha kisasa kikiwamo cha green house na umwagiliaji, Tanzania badi tuna ardhi kubwa lakini tatizo letu tunalima kwa kuhama hama  badala ya kutumia eneo dogo kwa kufuata kanuni na mbegu bora, sijajua kama tatizo ni elimu kushindwa kufika kwa wananchi.


“Tunawaomba wananchi wa kanda ya Ziwa na wale wanaofanikiwa kufika hapa Nyamhongolo waje hapa ili  tupeane maelezo ya kutosha  ikiwamo bei ya trekta, tunaweza kukukopesha na ukafanyia kazi na kulipa kidogo kidogo, lengo letu ni sawa na mpango wa Serikali kuona kilimo kinawanufaisha wakulima,”alisema.


Awali,Serikali ilisema  sera iliyopo ya sekta ya kilimo inayotumika kwa sasa  ndiyo cha chanzo cha wakulima kuwa masikini kutokana na kuwatumikisha wananchi kuilisha nchi na  matajiri huku wakiwa wanakabiliwa na changamoto kubwa.


Kutokana na hali hiyo ilisema sera hiyo imepitwa na wakati ambapo wizara ya kilimo  imelazimika kuanza kuipitia upya  na kuondoa  changamoto  na vikwazo kwa wakulima  ikiwa lengo ni kuihuisha  sekta hiyo kutoka kilimo cha kujikimu na kuwa cha biashara kwa kuruhusu uwepo wa uwekezaji mkubwa.


Kauli hiyo imetolewa  na Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe  wakati akifungua sherehe za wakulima  na maonyesho ya kilimo (Nanenane) katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza ambapo aliwapiga marufuku wakuu wa wilaya na mikoa kuwazuia wakulima kuuza chakula chao kwa kuhofia uwepo wa njaa.


 “Hatuwezi kujenga viwanda wakati wakulima ni masikini wa kutupwa, ni lazima tuwawezeshe kwa kutengeneza mazingira ya watu kunufaika na kilimo chao sambamba na kuwa na soko la uhakika, ndio maana leo hii kama wizara tumeanza kupitia sera ya kilimo na kuondoa changamoto  na  vikwazo vilivyokwekwa .


“Sera iliyopo imepitwa na wakati  kabisa,  inawaumiza wakulima   na kuwafanya kubaki  kila mwaka kuilisha nchi na matajiri huku wao wakibaki na umasikini wao huku kukiwapo na utitiri wa taasisi nyingi ambazo ukichunguza zimeanzishwa kwa lengo la kuwakandamiza wakulima, hii haiwezekani kama wizara tumeanza kuangalia ni taasisi gani zinatkiwa kufutwa na kubaki  chache .


“Fedha ambazo zilikuwa zikielekezwa kwenye utitiri wa taasisi hizo, zitaelekezwa katika mfuko maalum amboyo  wizara tunatarajia kuanzisha  na kazi ya mfuko huo ni kufidia mkulima pale inapotokea mtikisiko wa bei katika soko la dunia, kama serikali hatuna uwezo wa kuthibiti bei ya soko la dunia lakini mfuko huo ndio utakaokuwa na kazi ya kutafuta pesa kwa ajili ya kuwafikia wakulima,”alisema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.