• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkoa wa Mwanza kujenga Shule mpya za Sekondari 11 na madarasa 983 mwaka huu

Posted on: October 24th, 2022

Jumla ya Shule Mpya 11 na vyumba vya madarasa 983 vinatarajiwa kukamilika Disemba mwaka huu Mkoani Mwanza tayari kwa ajili ya kutumika na wanafunzi wa kidato cha kwanza watakaoanza masomo mwaka 2023.

Afisa Elimu wa Mkoa wa Mwanza Mwalimu Martin Nkwabi akizungumza leo Ofisini kwake na Vyombo vya Habari amesema Mkoa huo umepokea zaidi ya Shs Bilioni 19 ambazo zimeelekezwa kukamilisha ujenzi huo.

"Tangu kuanza mpango wa elimu bure mwaka 2016 Mkoa wa Mwanza umevunja rekodi tangu kupata Uhuru kwa kuwa na idadi ya wanafunzi 105,864 waliohitimu Elimu ya Msingi mwaka huu," amesema Afisa Elimu.

Mwalimu Nkwabi amebainisha kuwa kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza zinajengwa Shule hizo ambazo kila moja itagharimu Shs Milioni 600 na zingine tayari zimepata usajili.

"Tumejipanga vizuri kwa ajili ya wanafunzi hao hata kama wote watafaulu uwezo wa kusoma katika mazingira bora upo kutokana na mkakati uliopo wa kuboresha sekta ya elimu Mkoani hapa," amesisitiza Nkwabi

Aidha, amesema Mkoa huo umejenga Shule ya kisasa ya Sekondari ya Wasichana Wilayani Magu itakayochukua wanafunzi elfu moja kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita iliyogharimu Shs Bilioni 4 ambayo itakamilika kabla ya Disemba 15 mwaka huu.

Nkwabi ametoa rai kwa Maafisa elimu wote Wilayani kuhakikisha wanasimamia kwa weledi miradi hiyo ya ujenzi kwa kujiridhisha imekuwa na ubora kabla ya kuruhusu malipo kufanyika.

Serikali ya awamu ya Sita  chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa fedha  kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 8000 nchi nzima.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.