• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MONDULI YAIMWAGIA SIFA MWANZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: January 10th, 2025

MONDULI YAIMWAGIA SIFA MWANZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO


Halmashauri ya wilaya ya Monduli wapo Mkoani Mwanza kwa ziara ya mafunzo hususani wilayani Nyamagana katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza ambapo wamepikwa kwa siku 3 kwenye namna gani wanatekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi.

Akiongea kwa bashasha, Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Festo Kiswaga amempongeza Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa usimamizi mzuri wa miradi uliofanikisha wao kujifunza kwa kina na mna bora ya kuendeshesha halamshauri kwenye eneo hilo.

Amesema, wamejifunza mengi kwenye ziara hiyo hususani mradi wa Vizimba wa Vijana walioutembelea kwenye mwalo wa Luchelele katika kata ya Nyegezi kwani vijana hao wamewezeshwa fedha nyingi na wameendelea kusimamiwa na kupewa muongozo uliniandikia.


Ameongeza kuwa uimara wa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana kwenye usimamizi wameuona kwa macho kwani walikua naye katika ziara hiyo na ameonesha umahiri wa kuelezea fedha na muda halisi wa utekelezaji wa mradi jambo lililowapa funzo ya kwamba Mkurugenzi na Wakuu wa Idara wapo naye sambamba wakati wote.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Mkoa huo unatekeleza miradi lukuki kwenye ardhi na majini ikiwa ni katika kuhakikisha wananchi wanakua salama na uhakika wa miundombinu ya maendeleo.

Mhe. Mtanda ametaja baadhi ya miradi inayotekelezwa na Serikali kama Ujenzi wa Meli ya kisasa na Vivuko kwa ajili ya kusafirisha abiria kwenye visiwa pamoja na Soko la Kisasa, Reli ya SGR, Hospitali na upanuzi wa bandari ya Mwanza Kaskazini na Uwanja wa Ndege ambao utapandishwa hadhi kuwa wa Kimataifa.

"Sasa hivi Mkoa wetu wa Mwanza unafanya mkakati wa kuhuisha masuala ya utalii na ndio maana wenzetu wa NSSF wamejenga hoteli ya kisasa kubwa kwa ajili kuhudumia wageni wa kimataifa" Amefafanua.


Aidha, ameongeza kuwa wana Mwanza wanaongozwa na umoja na ushirikiano ndio siri ya mafanikio na maendeleo ya kasi hivyo wana Monduli na hata Arusha wanapaswa kujikita kwenye ushirikiano.

Ziara hiyo imejumuisha Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri, Waheshimiwa Madiwani na baadhi ya Wakuu wa idara wa Halmashauri hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.