• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (PSLE 2019) kuanza kesho

Posted on: September 10th, 2019


Mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi kitaifa unatarajiwa kuanza hapo kesho tarehe 11 na kumalizika 12 septemba 2019, Mkoa wa Mwanza ni miongoni mwa mikoa iliyojiandaa vyema kuhakikisha mtihani huo unafanyika na kumalizika vizuri.

Akizungumza ofisini kwake Afisa elimu wa Mkoa wa Mwanza, Michael Ligola amebainisha kuwa jumla ya shule 949 kutoka mkoa wa Mwanza zinatarajia kufanya mtihani huo ambapo katika idadi hiyo shule 850 ni za mfumo wa Kiswahili na shule 99 ni za mfumo wa kiingereza.

Aidha Ligola amebainisha idadi ya wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mtihani huo katika mkoa wa Mwanza wameandaliwa vizuri na wapo tayari kwa ajili ya mtihani huo hapo kesho.

“Mtihani huu unatarajiwa kufanywa na jumla ya idadi ya wanafunzi wapatao 68,078 ambao katika idadi hii wanafunzi 32,134 ni wavulana na 35,944 ni wasichana,” Alisema Ligola.

Ligola amebainisha kuwa idadi ya wanafunzi wenye uoni hafifu na wasioona watakao fanya mtihani huu kutoka shule za mfumo wa kiingereza na mfumo wa Kiswahili nao pia wameandaliwa vizuri na wapo tayari kufanya mtihani huo kwani hakuna changamoto zitakazokwamisha kufanikisha kwa mtihani huo.

“Mtihani huu utahusisha wanafunzi wasioona 7 ikiwa wavulana ni 6 na msichana 1 pia wanafunzi 37 wenye uoni hafifu kutoka shule za mfumo wa kiswahili ikiwa wavulana 14 na wasichana 13 na upande wa shule za mfumo wa kiingereza ni wanafunzi 5 kati yao mvulana ni 1na wasichana 4,” Alisema Ligola.

Hata hivyo Ligola ameaisitiza kuwa vifaa vyote vya mtihani vimeshawasili na wanafunzi wote wako tayari kwa ajili ya kufanya mtihani huo.

“Tayari tumepokea vifaa vyote na hatuna upungufu wa aina yoyote kwa upande wa watahiniwa pamoja na wasimamizi,”

Awali Ligola alianza kwa kuwatakia kheri wanafunzi wote watakao fanya mtihani huo wa kuhitimu darasa la saba na kuwatia moyo kuwa watafanya vyema na kuleta heshima katika mkoa wa mwanza.

 “Ninawatakia kila la kheri wanafunzi wote wa darasa la saba katika mtihani wenu wa kuhitimu elimu ya msingi na ninaimani mmejiandaa vyema katika mtihani wenu na ni matumaini yangu kuwa mtafaulu vizuri na kuleta heshima katika mkoa wetu,”

Pamoja na hayo Ligola amewaomba wazazi wa wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wahakikishe wanafunzi hao wanafanya mtihani, pia ametoa onyo kwa wazazi wanaowashawishi watoto wao kufanya mtihani vibaya ili wasifaulu kuacha tabia hiyo, lakini pia amewataka wasimamizi kusimamia vizuri na kuacha udanganyifu katika mtihani ili kuweza kupata matokeo ya haki.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.