• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yajikita kutatua changamoto za Elimu

Posted on: October 27th, 2019


Mkoa wa Mwanza unakabiliwa na upungufu mkubwa wa miundombinu ya elimu, hali inayoufanya uongozi wa mkoa kuchukua hatua madhubuti ya kukabiliana na upungufu huo.

Hayo yameelezwa  jijini hapa na Afisa Elimu wa Mkoa wa Mwanza Mwl. Michael Ligola alipokuwa akiwasilisha taarifa ya hali ya elimu mkoa kwenye mkutano wa wadau wa elimu, kikao ambacho kilihudhuriwa pia na Wakuu wa wilaya, wenyeviti wa halmashauri, wakurugenzi watendaji kwa wilaya zote za mkoa.

Alisema kwa upande wa shule za msingi, Ligola alisema mkoa unakabiliwa na upungufu wa walimu 4,878 kati ya walimu waliopo 12,684 na kwa upande wa shule za sekondari zinahitaji jumla ya walimu 4,332 kwa masomo ya Sanaa na waliopo ni 4,077 na upungufu ni walimu kwa 389 katika halmashauri za Sengerema, Manispaa ya Ilemela na Magu.

“Kwa upande wa walimu wa sayansi, tuna upungufu wa walimu 1,765 kwa halmashauri zote na waliopo ni 1,351 na mahitaji ni walimu 3, 116,” alisema.

Kwa upande wa vyumba vya madarasa, Ligola alisema mkoa una upungufu wa vyumba vya madarasa 10,411, matundu ya vyoo 23,485 na nyumba za walimu 14,842

“ Kwa upande wa sekondari tuna upungufu wa vyumba vya madarasa 1,513, matundu ya vyoo 4,525, maabara 137 na nyumba za walimu 4,586,” alisema.


Aidha Ligola alisema kumekuwepo na mdondoko wa wanafunzi kwa ngazi mbalimbali za elimu kimkoa, ambapo kwa mwaka huu jumla ya wanafunzi 16,780 sawa na asilimia 19.8 ya walioandikishwa darasa darasa la kwanza mwaka 2013 hawakuhitimu elimu ya msingi.

“Sababu iliyosababisha mdondoko huo ni utoro unaosababishwa na umbali kufika shuleni, migogoro ya ndoa, utovu wa nidhamu, ajira za utotoni, ukosefu wa hosteli na mimba,” alifafanua.


Aliwataka wadau wa elimu kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kuchangia miundombinu ya elimu kwa madai kuwa serikali haiwezi kufanya kila kitu peke yake.


Kwa upande wao, wakuu wa wilaya zote wa mkoa wa Mwanza, ambao kila mmoja alikuwa akivutia upande wake, walisema watahakikisha wanaweka mikakati imara itakayosaidia kuongeza viwango vya ufaulu ili kuuwezesha mkoa wa Mwanza kuwa wa kwanza kitaifa.


Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Colnel Maghembe ambaye wilaya yake nafasi ya 115 kitaifa kutoka nafasi ya 130  mwaka jana na nafasi ya 4 kimkoa kutoka nafasi ya 8 kimkoa kwa mwaka jana, alisema siri ya mafanikio ya ushindi huo ni kujenga mazingira mazuri kwa walimu kwa kushirikisha jamii, wanafunzi na walimu.


Akiahirisha mkutano huo wa wadau wa elimu, Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela aliwataka viongozi wote wa wilaya kutobweteka na ushindi waliopata kwa mwaka, bali wawe na mipango kazi inayotekelezeka katika suala zima la elimu.


“Wakuu wa wilaya nendeni mkatatue changamoto za elimu kwenye maeneo na fundisheni vijana wetu uzalendo,” alisema.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.