• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh Abdallah Ulega awahakikishia Vijana Mwanza kupata mkopo wa Shs Bilioni 2.5

Posted on: August 20th, 2022

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewahakikishia Vijana wa Mwanza wanaojishughulisha na Miradi ya Ufugaji wa Samaki kwa njia ya Vizimba kupata fedha Tshs Bilioni 2.5 walizoomba kama mkopo kutoka Benki ya Kilimo.

Ametoa wito huo leo Agosti 19, 2022 wakati akizungumza na Vijana wanayojihusisha na Miradi hiyo na amemuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa huo kufika Dodoma akiwa na vielelezo vya andiko la mkopo huo ili akutane na Wataalamu wa Wizara yake ili kukamilisha kupatikana fedha hizo.

"Natambua ugumu wa Benki kutoa fedha hizo lakini sasa nitatumia njia nyingine kwa kumuhusisha Waziri wa Mifugo na Wataalamu wengine kufanikisha kupatikana fedha hizo mwezi wa tisa" amesisitiza Naibu Waziri.

Amesema amevutiwa na utaratibu uliowekwa na Mkoa katika kufanikisha Miradi ya Ufugaji wa samaki kuwa bora kwa njia ya Vizimba kwa baadhi ya Vikundi vilivyopo Wilaya nne alizotembelea za Sengerema, Ukerewe, Ilemela na Nyamagana.

"Nimesikia kikundi cha Ufugaji samaki cha Ilemela walikwenda Uganda kwa ziara ya mafunzo, hii ndiyo njia sahihi ya kuongeza tija katika Miradi hii," amesema Mhe. Ulega.

Awali akizungumzia hali ya uzalishaji Mali Kwa Makundi ya Vijana Mkoani Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na uzalishaji Emil Kasagara amesema Ufugaji wa Samaki kwa njia ya Vizimba umekuwa na faida kutokana na Vijana wengi kufaidika na kuondokana na kukaa vijiweni kwa kukosa ajira.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amebainisha wamejipanga kuhakikisha wanatimiza ndoto za Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kuona uchumi wa bluu unawanufaisha Vijana na makundi mengine.

Amezitaka Taasisi zote za fedha za Serikali na mamlala zingine za utoaji vibali kuacha kuwawekea vikwazo visivyo vya lazima wanaofika kwa mahitaji ya Miradi yao.

Naye, Mbunge wa viti Maalum Vijana Mkoa wa Mwanza Mhe. Ng'wasi Kamani amesema rasilimali ya Maji ya Ziwa Victoria itazidi kuwanufaisha hasa Makundi ya Vijana na kuiomba Serikali kuzidi kuwaongezea kiwango cha Mikopo ya fedha.

Naibu Waziri Ulega amekuwa na ziara ya siku nne Mkoani Mwanza kukagua Miundombinu iliyo chini ya Wizara yake.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.