• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

OFISI YA MKUU WA MKOA ITAHAKIKISHA HAKI ZOTE ZA WATU WENYE ULEMAVU ZINALINDWA NA KUTEKELEZWA-RC MAKALLA

Posted on: July 6th, 2023

OFISI YA MKUU WA MKOA ITAHAKIKISHA HAKI ZOTE ZA WATU WENYE ULEMAVU ZINALINDWA NA KUTEKELEZWA-RC MAKALLA


*Awaahidi kutengewa maeneo ya biashara maeneo ya Masoko*


*Ashauri Mwanza kwenda kujifunza soko la Machinga Complex kuhusu kuwatengea vizimba watu wenye ulemavu*


*Usalama wao ndiyo kipaumbele cha kwanza*


*Ampongenza Mbunge wa viti Maalum Mhe. Khadija Shaaban kwa uwajibikaji mzuri kwa makundi maalum*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amewakikishia watu wenye ulemavu Mkoani humo kuzilinda na kuzitekeleza haki zao zote wanazostahili kama watu wengine likiwemo kutengewa maeneo yao ya biashara kwenye Masoko na usalama wao kwa ujumla.

Amesema hayo leo wakati wa mazungumzo ya pamoja na wawakilishi wa Vyama vya watu wenye ulemavu na kula nao pamoja chakula kwenye ukumbi wa Mwanza Hotel ambapo amesisitiza hakuna nafasi ya mtu yoyote kubaguliwa kutokana na kasoro yake ya kimaumbile na wachache wanaofanya hivyo watambue mkondo wa sheria utawapitia.

"Nimekaa hapa nimewasikiliza wote mnaowawakilisha wenzenu changamoto zote mnazopitia,narudia kusema nimeyapokea na nitakwenda kuyafanyia kazi kasoro tu yale ya kisera na sheria,"CPA Makalla.

Amesema alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Da r-e.s-Salaam ametengeneza mazingira mazuri kwenye soko la Machinga Complex kwa kuwatengea maeneo rasmi watu wenye ulemavu, hivyo na kutaka Mkoa wa Mwanza ujifunze kwa mpango huo.

Mhe. Makalla amesema amesikia kilio cha Vyama hivyo kukosa Ofisi za kufanyika kazi hivyo suala hilo ameagiza litekelezwe haraka kwenye majengo yote ya Taasisi za Serikali wapatiwe nafasi.

"Tayari Rais wetu Dkt.Samia Suluhu ameshatoa maagizo hayo hivyo hakuna sababu ya kusua sua au kujadiliana wahusika wote mhakikishe viongozi hawa wa vyama vya walemavu wanapatiwa Ofisi za kufanyia shughuli zao,"amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha amewatahadharisha wale wote wanaotoa lugha zisizo na staha kwa watu wenye ulemavu wakiwemo Albino kuwacha tabia hiyo na wanaowakataa kuingia kwenye vyombo vya usafiri LATRA na RTO wawachukulie hatua za kisheria

"Mhe.Mkuu wa Mkoa huu ni utaratibu niliojiwekea wa kuzunguka mikoani na kukutana na makundi maalum ninayoyawakilisha Bungeni,kusikiliza changamoto zao na kwenda kuzisemea ili ufumbuzi upatikane,"Khadija Shaaban maarufu kama Keisha,Mbunge wa viti maalum.

"Sisi kama wawakilishi wa wananchi tuna wajibu wa kupigania usawa wa wananchi wote,na kwa kupitia Mkutano huuu tunazidi kupata mengi ya kujifunza na kuyatekeleza," Mhe.Stanslaus Mabula,Mbunge wa Nyamagana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.