• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

PAMBA JIJI FC YAPATA MAPOKEZI YA AINA YAKE, JIJI LAZIZIMA KWA SHANGWE BAADA YA KUFUZU LIGI KUU MSIMU UJAO

Posted on: May 1st, 2024

PAMBA JIJI FC YAPATA MAPOKEZI YA AINA YAKE, JIJI LAZIZIMA KWA  SHANGWE BAADA YA KUFUZU LIGI KUU MSIMU UJAO


Furaha, vifijo, nderemo na kila aina ya shamrashamra vimetawala wakati wa mapokezi wa timu ya soka ya Pamba Jiji FC wakati ikiwasili ikitokea Arusha baada ya kufuzu kucheza ligi kuu msimu ujao.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda aliipokea timu hiyo eneo la Misungwi na kuambatana na timu hiyo maeneo mbalimbali kabla ya kuingia eneo rasmi la tukio.

Funga kazi na shughuli mbalimbali kulazimika kusimamia kwa muda ilikuwa mara baada ya timu hiyo kuingia viunga vya Jiji la Mwanza na kuanza kukatiza kwenye barabara za Pamba, Buzuruga Nyasaka, Makongoro hadi kuingia uwanja mkongwe wa Nyamagana.

Mhe. Said Mtanda aliyeonekana kuzidiwa kwa furaha amebainisha kuwa sasa ni wakati wa kuiweka timu ya Pamba Jiji katika hadhi ya ligi kuu huku akitangaza rasmi dimba la Nyamagana kuwa la nyumbani kwa timu hiyo.

"Mkurugenzi wa Jiji awali ya yote nakupongeza sana nimeona juhudi zako sasa nataka kuona majukwaa kwenye uwanja huu na taa ili mechi za usiku zirindime humu," amehimiza mkuu huyo wa Mkoa mkereketwa wa soka.

Amesema ligi kuu ina hadhi yake, Pamba Jiji Ina historia nzuri katika ramani ya soka, ni lazima iwe na majengo yake ya klabu na hosteli za kisasa.

"Mechi zote kasoro za Simba na Yanga zitapigwa hapa Nyamagana,huu ni miongoni mwa viwanja bora unahitaji marekebisho kidogo na tutaishuhudia timu yetu ikisukuma gozi la ng'ombe humu huku timu zikitoka na vichapo," amesema Mtanda huku akishangiliwa na umati wa mashabiki waliofu rika uwanja I hapo.

Mkuu huyo wa Mkoa ameuagiza uongozi wa Jiji la Mwanza unaomiliki timu hiyo kuhakikisha unaunda safu imara ya watu wa kuliongoza timu hiyo hhuku wachezaji wa zamani nao wakipewa nafasi za heshima za kuingia uwanjani na ushauri kwa Pamba Jiji.

"Hongera sana Mkuu wetu wa Mkoa umetuheshimisha sana,pia hongera zake mtangulizi wako comrade Amos Makalla wote kwa pamoja mmefanya kazi kubwa",Amina Makilagi Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana.

Awali, timu hiyo maarufu kama TP Lindanda mara baada ya kupokelewa Wilayani Kwimba eneo la Hungumalwa wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Ng'wizalubi Lidigija.

"Hutushuki tena,..Pamba oyeeee sasa tumepata burudani tuliyoikosa miaka mingi karibuni majembe wetu kazi tumeiona asanteni," ni kauli za mashabiki wa soka walipopaza sauti kwa wachezaji wa Pamba Jiji FC.

Pamba Jiji  FC ilianzishwa rasmi mwaka 1984 na kufuzu ligi kuu kwa mara ya kwanza mwaka 1984 kabla ya kushuka daraja mwaka 2000.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.