• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAIS SAMIA ATOA ZAIDI YA BILIONI 30 KUJENGA VIVUKO VIPYA MWANZA: RC MAKALLA

Posted on: January 10th, 2024

RAIS SAMIA ATOA ZAIDI YA BILIONI 30 KUJENGA VIVUKO VIPYA MWANZA: RC MAKALLA


*Amshukuru Mhe. Rais kwa kuboresha usafiri wa majini*


*Awataka TEMESA kumsimamia mkandarasi kukamilisha ujenzi*


*Awapongeza Songoro Marine kwa uhodari na kujenga boti za uokozi Ukerewe*


*Amezitaka Halmashauri kutatua changamoto za vituo vya ufuatiliaji*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Januari 10, 2024 amekagua ujenzi wa vivuko vipya vitano vinavyojengwa kwenye karakana ya Songoro Marine Wilayani Ilemela kwa zaidi ya Bilioni 30.


Akiongea na uongozi wa mkandarasi huyo pamoja na wasimamizi (TEMESA) Makalla ametumia wasaa huo kumpongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha hizo kujenga vivuko vipya vitakavyoimarisha usafirishaji ziwani.

Amesema, awali wananchi waishio kwenye visiwa walipata shida kusafiri kwa kutumia mitumbwi jambo lililohatarisha usalama wao lakini kukamilika kwa vivuko hivyo kwa pamoja mwishoni mwa mwezi Machi 2024 kutaimarisha usafiri.


"Wananchi wetu siku za nyuma walitumia vivuko visivyo na uhakika, uwekezaji huu mkubwa wa Mhe. Rais wa zaidi ya Bilioni 30 kujenga vivuko hivi vipya utasaidia kuimarisha usafiri kwenye visiwa hususani Ukerewe, Magu na Sengerema." Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amempongeza na kumshukuru mkandarasi Songoro Marine Co. Ltd kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwa uaminifu na akawataka TEMESA kulipa fedha kwa wakati na kusimamia usiku na mchana ili kazi ikamailike kwa wakati kwa mujibu wa mkataba.


Awali, Mkurugenzi wa kampuni ya Songoro Marine Major Songoro ameahidi kujenga kwa kasi na kukamilisha kwa wakati kwa mujibu wa mkataba ili wananchi wanaovisubiri wapate uhakika wa usafiri kwenye maeneo na kwamba vyote kwa pamoja vitakamilika kabla ya mwezi Mei 2024.

"Mhe. Mkuu wa Mkoa tunaendelea na ujenzi wa vivuko vya Rugezi - Kisorya kwa zaidi ya Milioni 892, Ijinga -Kihangara kwa Bilioni 5, Bwiru -Bukondo kwa Milioni 677, Nyakalilo-Kome kwa zaidi ya Bilioni 8.5 pamoja na Buyagu-Mbariika kwa zaidi ya Bilioni 3.5 na tutakamilisha kwa mujibu wa mkataba." Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.