• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA ATANGAZA MATOKEO YA DARASASA LA SABA KANDA YA ZIWA, MWANZA YANG'ARA

Posted on: June 13th, 2024

RAS BALANDYA ATANGAZA MATOKEO YA DARASASA LA SABA KANDA YA ZIWA, MWANZA YANG'ARA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana leo Juni 13, 2024  ametangaza matokeo ya Mtihani wa Utamilifu kwa darasa la Saba Kanda ya ziwa huku Mwanza ikiing'ara kwa ufaulu wa asilimia 84.6 kwa jumla ya wanafunzi 219,655 waliofanya mtihani huo.

Akitangaza matokeo hayo kwa niaba ya Makatibu Tawala wa Mikoa 5 ya Kanda ya ziwa, Elikana amebainisha kuwa nafasi ya pili imekwenda Mkoa wa Simiyu waliopata ufaulu wa 81%  ikifuatiwa na Geita wenye ufaulu wa 72.6%,wakati Kagera wakiwa nafasi ya nne ya ufaulu wa 62.4% na Mara wakiwa na 52.8%.

"Rai yangu kwenu Maafisa Elimu mliohudhuria hafla hii tuzidi kuongeza bidii kwani takwimu zinaonesha masomo matatu ya Hisabati, Kiingereza na Sayansi na Teknolojia wanafunzi hawajafanya vizuri, tulibebe jukumu hili kabla ya wanafunzi hawajafanya mtihani wao wa kumaliza elimu ya msingi Septemba mwaka huu", amesisitiza Balandya.

"Tunapaswa kuiunga mkono Serikali ya Rais Samia ambayo imeleta zaidi ya Tshs. bilioni 16 kwa  mikoa ya Kanda ya ziwa (2023/24) Mwanza ikipata shs bilioni 4.3 kwa ajili ya kuboresha elimu ukiwemo ujenzi wa shule mpya, nyumba za walimu na matundu ya vyoo," Balandya.

Akitoa taarifa fupi ya mtihani huo wa Utamilifu kwa niaba ya Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Afisa Taaluma Mkoa anayeshughulikia elimu ya Sekondari Aisa Rupia amesema mtihani huo umefanyika Mei 22 hadi 23 mwaka huu ikijumuisha Halmashauri 37 yenye jumla ya shule 4205 kati ya hizo 3834 za Serikali na 371 za binafsi.

"Ndugu Mwenyekiti watahiniwa wamepimwa katika masomo sita ambayo yanafundishwa kulingana na mtaala mpya ulioboreshwa ambayo ni Hisabati, Kiingereza,Kiswahili,Sayansi na Teknolojia,Maarifa ya Jamii na stadi za kazi, na Uraia na Maadili,"Rupia

Wakati huo huo Elikana, leo asubuhi Ofisini kwake amekutana na uongozi wa Shirika linalowasaidia watoto wa kike elimu ya stadi za maisha kuanzia kidato cha kwanza, CAMFED TANZANIA ambao watafanya shughuli hiyo kwenye wilaya za Magu, Misungwi, Kwimba na Halmashauri ya Buchosa.

Katika mazungumzo mafupi mtendaji huyo wa Mkoa ameutaka ujumbe huo ambao ni walimu kitaaluma kuweka mkazo wanafunzi kuyapenda na kuyachangamkia masomo ya Hisabati na Sayansi.

Kiongozi wa kundi hilo Mussa Siame amesema mwaka huu wamepangiwa maeneo hayo na changamoto watakazo zibaini wataziwasilisha Tamisemi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.