• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AWATAKA WATENDAJI KUTUMIA MIFUMO KUBORESHA HUDUMA

Posted on: December 5th, 2023

RAS MWANZA AWATAKA WATENDAJI KUTUMIA MIFUMO KUBORESHA HUDUMA


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amewataka watendaji kwenye mamlaka za Serikali za mitaa kutumia fursa ya uwepo wa mifumo kuboresha huduma zao katika kuhudumia wananchi.

Ametoa wito huo leo wakati wa kikao kazi cha Maafisa TEHAMA, usimamizi wa fedha, mipango na usimamizi na ukaguzi kutoka Mikoa 10 ya kanda ya Ziwa, kaskazini na kati kinachoratibiwa na TAMISEMI chini ya ufadhili wa mradi wa USAID PS3+.

Balandya amesema huko nyuma TAMISEMI ilisimamia mifumo yote lakini sasa wataalamu wapo kwenye kila mamlaka inayotumia hivyo ni fursa kwa wataalam hao kuitumia katika kuboresha huduma wanazotoa kwa jamii.

"Yatumieni mafunzo haya ya siku tano vizuri kwani ni wajibu wetu kusimamia mifumo kutekeleza shughuli za wananchi kwa ufanisi kwa kuboresha huduma tunazotoa" Amesema Balandya.

"Hii ni mara ya pili tunawawezesha maafisa wa sekretarieti za mikoa ili waweze kusimamia utekelezaji wa mipango na bajeti ili nao wakasimamie vizuri Halmashauri kwa kutumia mifumo" Amesema Ndugu Johnson Nyingi kutoka TAMISEMI.

Naye, ndugu Sono Kusekwa kutoka USAID PS3+ mradi wa miaka mitano unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani na kutekelezwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la watu wa Marekani (USAID) unaowezeshwa na Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) amesema shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha mifumo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.