• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AAGIZA UANDALIWE MPANGO MKAKATI WA KUKUZA SEKTA YA UTALII MKOA WA MWANZA

Posted on: November 30th, 2023

RC MAKALLA AAGIZA UANDALIWE MPANGO MKAKATI WA KUKUZA SEKTA  YA UTALII MKOA WA MWANZA.


*Amuagiza Katibu tawala Mkoa kuandaa kikosi kazi cha kuandaa mpango huo ukihusisha  wadau wa utalii


*Awataka kutumia miundombinu inayojengwa kuboresha utalii Mkoani humo*


*Abainisha kuwa mwezi Disemba mkataba wa Ujenzi wa Jengo la abiria uwanja wa Ndege Mwanza utasainiwa*


*Asema Mwanza ina mazingira mazuri ya Utalii wa Ziwa na ipo jirani na Hifadhi za Taifa kama Serengeti*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wadau wa utalii Mkoani humo kutumia fursa ya uwepo wa mazingira rafiki ya ukanda wa ziwa, ujirani na hifadhi za Taifa na uwepo wa vivutio vya utalii kuboresha sekta hiyo kwa kuwekeza kwenye utalii kwa manufaa ya Taifa.


CPA Makalla amesema hayo mapema leo Novemba 30, 2023 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati wa kikao kazi na wadau wa utalii kilichokutuna mahsusi ili kujadili na kuweka mpango mkakati wa kuboresha sekta hiyo kwa kutumia mazingira rafiki kwenye ukanda huo uliobarikiwa.

Katika kuhakikisha suala hilo Mkuu wa Mkoa amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kuunda kikosi kazi cha kuandaa mpango mkakati huo kikihusisha wataalam kutoka makundi mbalimbali ili kutoka na andiko linalojibu kila swali linalohusu namna gani sekta ya utalii mkoani humo itaboreshwa kwa manufaa ya wana Mwanza na Taifa kwa ujumla.


Amesema uwepo wa ziwa la kihistoria la Victoria, kufikika kwake kwa urahisi na hifadhi za Taifa kama Saanane, Burigi Chato, Rubondo, Rumanyika-Kagera na Serengeti pamoja na uwepo wa vivutio vya kitalii vya kihistoria kama Jiwe linalocheza lililopo Kisiwani Ukerewe, Jengo la Kijerumani la Gunsert na Bujora kunapaswa kusaidia kukuza sekta hiyo.

"Kwa takwimu zilizopo za idadi ya watu kuwa ni Mkoa wa pili, uwepo wa mifugo mingi, uvuvi, kilimo na uwanja wa ndege wa Mwanza ambao unaboreshwa ni ishara tosha kuwa wadau wakijipanga na kuchangamkia fursa zilizopo uchangiaji wa pato la Taifa utapanda na Mwanza itaongoza", amesisitiza.


Katika kuboresha utalii, Makalla amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu kama ujenzi wa daraja kubwa la Kigongo-Busisi, Meli ya MV Mwanza pamoja na Bandari, Reli ya kisasa na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza pamoja na ujenzi wa jengo la abiria la kisasa ambapo mwezi Disemba mkataba wa ujenzi utasainiwa.


Halikadhalika, Makalla amewataka wataalam hususani kwenye Halmashauri kuweka nia ya kuboresha utalii, kuanisha vivutio vilivyopo na miundombinu inayotakiwa kama mahoteli yenye hadhi na kujipanga na mikakati ya kutenga maeneo yenye hadhi kuendana na utalii ili kujihakikishia kukuza sekta hiyo na kumuunga mkono Rais Samia ambaye amejipambanua kuitegemea sekta hiyo.


"Ndugu viongozi ni lazima tuthubutu kushawishi watu wenye mahoteli na kampuni za kusafirisha watalii, sekta binafsi lazima ihamasishwe, vyuo vikuu na vya kati lazima vichangie kwenye kuwajengea uwezo rasilimali watu na kuhakikisha wanachangia ukuaji wa sekta ya utalii." Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.