• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AKIPONGEZA CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA KUJENGA CHUO CHAKE MWANZA

Posted on: December 7th, 2023

RC MAKALLA AKIPONGEZA CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA KUJENGA CHUO CHAKE MWANZA


*Aahidi uwepo wa maji ya kutosha kwenye eneo lake la ujenzi baada ya Mradi Mkubwa wa maji kukamilika*


*Akitaka chuo kuipa kipaumbele Mwanza kutokana na kukua kiuchumi*


*Wahitimu watakiwa kuwa wabunifu kupitia taaluma yao kujiajiri wenyewe*


*Atangaza fursa za kiuchumi Mwanza mara baada ya miradi ya kimkakati kumalizika*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amekipongeza Chuo cha usimamizi wa fedha IFM kwa hatua ya kujenga chuo chake  na kuahidi changamoto ya maji eneo la ujenzi itamalizika hivi karibuni kutokana na mradi wa maji Butimba kukamilika.

Akizungumza leo na wahitimu wa ngazi mbalimbali katika mahafali ya 49 ya Chuo cha usimamizi wa fedha IFM kampasi ya Mwanza na Simiyu yaliyofanyika ukumbi wa Rock City Mall, Mkuu huyo wa Mkoa amesema chuo hicho kuwa na majengo yake sasa itakuwa na wigo mpana wa kuwachukua wanafunzi wengi na hasa mahitaji makubwa ya wataalamu wanaohitajika Mkoani humo.

"Ndugu Mwenyekiti wa Baraza la uongozi Prof. Emmanuel Mjema, Mkoa wa Mwanza una miradi mingi ya kimkakati na unachangia kwa kiasi kikubwa pato la Taifa,hivyo wataalamu bora kwa upande wa fedha na uchumi watahitajika kutoka Chuoni kwako," CPA Makalla.

Aidha, amewataka wahitimu hao kwenda mtaani kuwa chachu ya mageuzi ya kiuchumi ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla na siyo vyeti hivyo kwenda kuvifungia kabatini.

"Ni lazima tutambue mara baada ya kutoka hapa suala la ajira bado ni changamoto, hivyo miende mkawe wabunifu wa kujiajiri wenyewe na hasa fursa nyingi za kiuchumi zilizopo Mkoani Mwanza kuanzia Utalii na uchumi wa bluu,"amefafanua Mkuu huyo wa Mkoa wakati anazungumza na wahitimu hao.

CPA Makalla amesema Mkoa wa Mwanza umejaliwa miradi mingi ya kimkakati kuanzia mradi wa reli ya kisasa SGR, Daraja la JP  Magufuli,u uenzi wa Meli ya Mv Mwanza pamoja na ujenzi wa uwanja wa ndege wa kisasa, miradi yote hiyo itakapo kamilika itahitaji wataalamu na pia fursa za kujiajiri zitakuwepo kwa wingi.

"Ndugu mgeni rasmi Chuo chetu cha IFM kimezidi kupiga hatua na sasa tuna jumla ya kampasi tatu Mwanza,Dodoma na Simiyu na sasa tupo mbioni kufungua kampasi ya nne huko Mkoani Geita,lengo ni kutoa wataalamu bora hapa nchini," Prof.Emmanuel Mjema,M/kiti wa Baraza la uongozi chuo cha usimamizi wa fedha IFM

Akizungumzia maendeleo ya Chuo hicho Mkuu wa chuo cha IFM Prof. Josephat Mtoto amebainisha walianza na wanafunzi 72 mwaka 1992 na sasa wamepiga hatua kwani mwaka 2022-23 wamekuwa na jumla ya wanafunzi 15,000.

Jumla ya wahitimu 564 wamehitimu masomo yao ya ngazi mbalimbali kuanzia astashahada,shahada na shahada ya uzamili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.