• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA PAMBA JIJI FC KUJITUMA NA KUPATA MATOKEO MAZURI UWANJANI

Posted on: October 13th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA PAMBA JIJI FC KUJITUMA NA KUPATA MATOKEO MAZURI UWANJANI


*Asema hafurahishwi na mwenendo wa sasa wachezaji kutokujituma na kupata matokeo yasiyoridhisha*


*Awataka kubadilika kuanzia mchezo wao ujao*


*Awahaidi changamoto zao kuzifanyia kazi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wachezaji wa Pamba Jiji FC kujitafakari haraka kabla ya mchezo wao ujao wa Ligi ya Championship  kutokana na matokeo yasiyoridhisha.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mlezi wa timu hiyo amezungumza leo Oktoba 10, 2023 mara baada ya mazoezi yao kwenye uwanja wa Nyamagana, amebainisha  hali halisi ni wachezaji kutojituma uwanjani ndiyo maana timu imepata matokeo yasiyoridhisha na kushika nafasi ya saba na pointi 7.

"Nimezungumza na makocha kadhaa wa Ligi ya Championship wanasema wazi kabisa tumefanya usajili bora hadi dawati la ufundi lakini changamoto tuliyonayo ni kucheza chini ya kiwango na tusipo badilika haraka itatugharimu", CPA Makalla.

Ameongeza kuwa lengo ni timu kucheza Ligi kuu msimu ujao ndiyo maana imefanyiwa maandalizi mazuri ya kutoka kuchangiwa bakuli na sasa inamilikiwa na Halmashauri ya Jiji na endapo hakutakuwa na mabadiliko juhudi za haraka za kuongeza nguvu za wachezaji kutoka nchi jirani zitafanywa wakati wa dirisha dogo.

CPA Makalla akiwa ameambatana na baadhi ya wachezaji wa zamani wa Pamba FC akiwemo Fumo Felician naye alipata wasaa wa kuwatia shime kucheza kwa bidii kama walivyofanya wao miaka ya nyuma.

"Tambueni mnaichezea timu yenye jina kubwa hapa nchini,huu ni wakati wa kutupa matokeo mazuri kutokana na mazingira mliyonayo,sisi miaka ya nyuma maslahi hayakuwa makubwa zaidi ya kucheza kwa uzalendo na kuupambania Mkoa". Fumo Felician, mshambuliaji wa zamani,Pamba FC


"Mhe.Mkuu wa Mkoa tumekusikia ila changamoto inayotukabili ni timu nyingi kutupania kila tukicheza nazo, tunatambua matokeo haya hayawafurahishi mashabiki wa soka tunawaahidi kujirekebishia,"Jerry Tegete,Nahodha wa timu.

Pamba Jiji FC baada ya kucheza michezo 5 ikishinda miwili, imepoteza mmoja na kutoka sare, hata hivyo jumamosi hii itashuka uwanja wa nyumbani Nyamagana kupepetana na Green Warriors.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.