• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI UKARA WA ZAIDI YA BILIONI 4.5

Posted on: November 22nd, 2023

RC MAKALLA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI UKARA WA ZAIDI YA BILIONI 4.5


*Amshukuru Rais Samia kwa kuwaletea wananchi wa kisiwa hicho maji safi*


*Mradi huo wafikia asilimia 80 ya utekelezaji*


*Aahidi kufuatulia fedha za ukamilishaji wa kradi huo*


*Awasihi wananchi kuutunza mradi kwa manufaa ya muda mrefu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Novemba 22, 2023 ameweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Ukara unaotekelezwa na Mkandarasi M/S Halem Construction Company Limited kwa zaidi ya shs bilioni 4.5 chini ya usimamizi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Ukerewe.

Akizungumza na wananchi kwenye chanzo cha mradi huo Mhe. Makalla amemshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha hizo kwa ajili ya kuwapatia maji safi wananchi zaidi ya elfu 40 wa kisiwani humo ambao wataondokana na adha ya kuugua magonjwa ya tumbo na hatari ya kuliwa na Mamba.

Makalla amesema nia ya dhati ya Rais Samia kwa wananchi wake wa vijiji vinane ni lazima itimie na kwenye hilo atahakikisha anafuatilia fedha za mradi huo ili mkandarasi aweze kulipwa na amemtaka kuendelea na kazi na kuhakikisha anakamilisha mradi huo muhimu kwa jamii.

"Niwahakikishie kwamba kazi hapa haita simama, ninakwenda kulifanyia kazi suala la fedha za mradi huu na mkandarasi abaki eneo lake la kazi aendelee kwani atakua shuhuda na wananchi wataona mabadiliko makubwa muda si mrefu." Makalla.

Aidha, ametumia wasaa kuwapongeza wabunifu wa mradi huo kwa kutumia nishati ya jua ambayo itasaidia kupunguza gharama za uendeshaji na amewasihi wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo ili mradi wao uweze kujiendesha na kuwasaidia kwa muda mrefu.

"Kukamilika kwa mradi huu utakaosaidia wananchi kwenye vijiji 8 ni ishara ya kuondokana na maradhi ya tumbo na Rais Samia amedhamiria kuwafikia wananchi kwenye vijiji vyote 76 kwenye jimbo letu." Amezungumza Mhe. Joseph Mkundi Mbunge wa Ukerewe kwa niaba ya wananchi.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ukerewe Mhe. Ally Mambile amemshukuru Rais Samia kwa kuwajali wananchi wa vijiji vya Bwisya, Bukungu, Chifule, Chibasi, Nyang'ombe, Nyamanga, Kome na Bukiko na amebainisha kuwa Ilani ya chama hicho  anaitekeleza vema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.