• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awakumbusha Makarani wa Sensa kufuata taratibu

Posted on: August 24th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Adam Malima leo Agosti 24 ameendelea na ziara yake ya kukagua utekelezaji wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi leo ikiwa ni siku ya pili ametembelea Wilaya ya Sengerema Halmashauri ya Buchosa Kata ya Nyehunge.

Akizungumza na Karani wa Sensa katika moja ya kaya iliyopo Kata ya Nyehunge aitwaye  Lucy Lucas Lubala,  Mhe. Malima amesema  Makarani wa Sensa wanatakiwa kukadiria kaya watakazozihesabu  kwa siku ili  waruhusu watu waendelee na shughuli zao za kila siku.

" Karani kama jana umehesabu nyumba 25 leo unaweza kukadiria walau kaya 30 ili kaya zitakazobaki bila kufikiwa waalikwe kiubalozi, amesema Mhe.Malima.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe.Senyi Ngaga amesema  wamejiandaa vizuri kukabiliana na changamoto zozote zitakazojitokeza ili kufanikisha zoezi hilo.


Kwa upande wake Thomas Ngusa mshauri wa Kitongoji cha Senta Magharibi - Nyehunge amesema kwa upande wao walijigawa kiubalozi kwa hiyo hawakukaa kitongoji kizima nyumbani ili kusubiri Karani badala yake walipata maelekezo mazuri, wanakwenda ubalozi kwa ubalozi.

Baada ya maelezo ya Ngusa Mhe.Malima aliwapongeza wananchi na viongozi wa Kata ya Nyehunge kwa kuweka utaratibu wa kuwaachia wananchi kuendelea na shughuli zao badala ya kuwaambia wakae nyumbani kwao kusubiri Karani wa Sensa.

Hata hivyo, amewaomba wananchi wa Nyehunge kuendelea kutekeleza kikamilifu na kukumbushana kuhusu umuhimu wa kuhesabiwa kwani zoezi lilianza jana tarehe 23.8.2022 na linaendelea Nchi nzima kwa siku saba

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.