• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga fedha za Lishe kwa wakati

Posted on: February 10th, 2023


MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amewaagiza  wakurugenzi  wa halmashauri zote mkoani humo kutenga na kuwasilisha  fedha za kutekeleza afua za lishe kwa wakati  ili kuepuka udumavu kwa watoto na kutengeneza kizazi cha watu wenye ufahamu.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Mkoani humo leo Februari, 10, 2023  wakati akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe na utambulisho wa mfumo wa M-Mama ambao lengo lake ni kuokoa maisha ya wanawake wajawazito, waliojifungua na watoto wachanga wanapokuwa na dharura za kiafya.

Agizo hilo la Mhe. Malima amelitoa baada ya Afisa Lishe wa Mkoa  huo, Sophia Lazaro kutoa taarifa ya utekelezaji wa afua za lishe kuanzia Julai hadi Desemba  2022 iliyobainisha kwamba miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na baadhi ya halmashauri kutotoa fedha zilizotengwa na serikali  kwa wakati ili  kuwezesha utekelezaji wa afua za lishe pia hazilingani na idadi ya watoto.

Ameziagiza  kila halmashauri kutoa fedha zote  za utekelezaji wa afua za lishe ifikapo Juni 30 mwaka huu kwa kufuata miongozo iliyopo kwani kila  kiongozi wakiwemo wakurugenzi wanapaswa kulipa kipaumbele suala la lishe ili kutengeneza taifa lenye watu watakaoendeleza taifa lakesho .

 “Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan  ameipa kipaumbele ajenda hii ya lishe tangu akiwa Makamu wa Rais na sasa ni Rais,  ili kutengeneza taifa bora la kesho kwa sababu watoto wanaokabiliwa na changamoto ya utapiamlo nao  wanategemewa kuendeleza nchi hapo baadaye ndiyo  maana serikali  inawajali ili waweze kuimarika kiafya, hivyo sitarajii kuona kiongozi yeyote hasa sisi ambao tunamsaidia Mhe.  Rais Samia Suluhu Hassan Kumkwamisha kwa namna  yoyote ile,”amesisitiza Mhe. Malima.

Katibu Tawala wa Mkoa huo, Balandy Elikana amesema” Kwa kipindi hiki ambacho kimebaki cha miezi minne ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2022/2023 tuchukue hatua zinazostahili kuhakikisha tunatekeleza makubaliano yaliyopo kwenye mkataba”.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.