• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima azindua msimu wa kilimo cha Pamba Mwanza kwa kuhimiza kilimo cha kisasa

Posted on: November 30th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amehimiza elimu zaidi kwa wakulima wa zao la Pamba ili malengo yatimie ya kumkomboa mkulima kiuchumi na Mkoa huo kuwa kinara wa zao hilo hapa nchini.

Akizindua  msimu wa kilimo cha Pamba Wilayani Sengerema kata ya Nyampande, Mkuu huyo wa Mkoa amesema lazima kuwepo na mabadiliko yenye tija kwenye Pamba kwa hekari moja kutoa kilo 500 hadi 600.

"Tuache kutumia kilimo cha uzoefu na badala yake tufanye kilimo cha kisasa kwa kuzingatia mbegu bora, mbolea ya MPK kutoka Minjingu na upandaji wa kutumia sentimita 60 mstari kwa mstari na mche kwa mche sentimita 30", amesisitiza Mhe. Malima

Aidha ametangaza vita kwa wale wote watakaobainika kusambaza pembejeo zisizo na ubora kwani wanachangia kumpa mzigo wa umasikini mkulima.

Kuhusu bei ya Pamba, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha mwelekeo mzima unategemeana na soko la Dunia na bei inabadilika kila wakati kutegemeana na wingi au upungufu wa upatikanaji wake na kuwataka wanasiasa kuwacha kutumia eneo hilo kujinufaisha kisasa.

Amesema, Serikali imechagua Mkoa wa Tabora na Katavi kuwa mzalishaji wa mbegu za Pamba ambazo zitatayarishwa kitaalamu ili ziwe na matokeo chanya kwa mkulima na mkakati wa kudhibiti bei ukiwa unafanyiwa kazi.

Mkoa wa Mwanza msimu huu umevuna kilo milioni 15 huku bei elekezi ikiwa Sh 1560 na kupanda hadi 2100.

Simiyu ndio Mkoa unaoongoza kwa uzalishaji wa zao la Pamba hapa nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.