• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATAKA MAUDHUI YA KUCHAGIZA MAENDELEO KWA VITENGO VYA MAWASILIANO YA SERIKALI

Posted on: July 17th, 2024

RC MTANDA ATAKA MAUDHUI YA KUCHAGIZA MAENDELEO KWA  VITENGO VYA MAWASILIANO YA SERIKALI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amevitaka vitengo vya Mawasiliano ya Serikali ngazi ya Mkoa na Halmashauri kuandika habari zenye maudhui bora ya kuhamasisha maendeleo na utatuzi wa kero za wananchi.

Mhe. Mtanda ameyasema hayo mapema leo Julai 17, 2024 baada ya kupokea kikombe na cheti cha ushindi wa nafasi ya pili kwa ngazi za Mikoa kilichotolewa na Waziri wa Habari Mhe. Nape Nnauye kwenye Kongamano la Habari lililofanyika jijini Dar es Salaam  Juni mwaka huu.

Mhe. Mtanda amesema katika kuhabarisha umma jamii inatamani kujua ni kitu gani Serikali inafanya kwa wananchi hivyo basi ni lazima vitengo hivyo vijikite katika kuelezea miradi ya maendeleo inayofanywa na Serikali kw ajili ya kuboresha huduma kama za maji, miundombinu ya barabara, elimu na afya.

Aidha, amesema ziara za viongozi zimekuwa na tija sana kwa jamii hususani usikilizaji kero za wananchi pamoja na kuzitatua kama ambavyo yeye binafsi anaendelea nazo hivyo vitengo vya mawasiliano vinapaswa kuonesha shida na madhila wanayopitia wananchi na jinsi gani zinatatuliwa.

Vilevile, Mhe. Mtanda ameagiza vitengo vya mawasiliano katika Halmashauri zote 8 za mkoani humo kuchapa kazi katika kuhakikisha wanahabarisha umma juu ya yote yanayoendelea kwenye maeneo yao huku akionesha kiu yake ya kupata habari za wananchi wanaoishi kwenye visiwa vya Ukerewe.

Akiwasilisha kikombe na cheti cha ushindi kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Paulo Zahoro amebainisha kuwa ushindi huo (nafasi ya 2 kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara) umetokana na uhabarishaji umma mzuri na akaahidi kuendelea kuboresha zaidi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.