• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWASHUKURU WANANCHI SENGEREMA KWA MAPOKEZI MAZURI YA KATIBU MKUU WA CCM

Posted on: August 14th, 2024

RC MTANDA AWASHUKURU WANANCHI SENGEREMA KWA MAPOKEZI MAZURI YA KATIBU MKUU WA CCM


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Wilaya ya Sengerema kwa kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi aliyewasili Mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Mhe. Mtanda ametoa shukrani hizo wakati alipokuwa akitoa salamu za Serikali ya Mkoa katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani Wilayani Sengerema, RC Mtanda amesema ni heshima kubwa kwa wananchi hao ambao wamejitokeza ikiwa ni kuashiria kushukuru kwa yale mengi mazuri yaliyofanywa na Chama hicho.

Aidha, Mhe. Mtanda amemuhakikishia Katibu Mkuu huyo usalama wa hali ya juu kwa kipindi chote atakachokuwepo katika Mkoa huo yeye pamoja na msafara wake, na kumtoa hofu kuhusu hali ya vurugu kwani jeshi la polisi Mkoani humo limejipanga kuhakikisha usalama unaimarishwa kwa kipindi chote

"Nimesimama hapa pia kukuhakikishia Katibu Mkuu kwamba hali ya ulinzi na usalama katika Mkoa wa Mwanza ni shwari kabisa kabisa, wewe na msafara wako mtafanya kazi yenu ya kisiasa katika Mkoa huu bila tishio lolote". RC Mtanda.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema serikali ya Mkoa wa Mwanza imejipanga kikamilifu kudhibiti vitendo vyovyote vinayoashiria uharibifu au uvunjifu wa amani, Aidha amemuomba Katibu Mkuu huyo kufikisha salamu  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ndani ya Mkoa wa Mwanza amefanya makubwa sana.

"...lakini niseme tu kwamba fedha za miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mwanza katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake ni zaidi ya tirioni 4.2 zimetumika kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo" amesisitiza Mtanda.

"Mhe. Balozi Nchimbi kesho kwa kuwa una mkutano mkubwa nitapata fursa ya kuainisha miradi mbalimbali ya kimkakati ambayo Rais wetu ameindeleza kwa mafanikio katika Mkoa wetu wa Mwanza. Ameongeza Mkuu huyo wa Mkoa.

Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa pia amemuhakikishia Katibu Mkuu huyo kuwa Chama cha Mapinduzi kuwa wanayo imani kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa hali ya usalama itakua kubwa na wananchi watashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo bila wasiwasi wowote ule.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.