Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA NSSF KUENDELEA KUSHUGHULIKA NA CHANGAMOTO ZA WASTAAFU

Posted on: May 28th, 2024

RC MTANDA AWATAKA NSSF KUENDELEA KUSHUGHULIKA NA CHANGAMOTO ZA WASTAAFU


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kuendelea kuwajengea uwezo wastaafu watarajiwa na kushughulika na utatuzi wa changamoto zinazowakabili wazee.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo Mei 28, 2024 wakati akizungumza na wastaafu watarajiwa ambao ni wanachama wa mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Mwanza.

Mtanda amesema kwa uzoefu aliokuwa nao kupitia uenyekiti wake wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii amebaini kuwa hifadhi za jamii haziwezi kujitenga na maslahi ya wazee kwa kuhakikisha wanajengewa msingi wa kutoa pensheni kwa kundi hilo.

"Semina hii inafanyika kwa madhumuni ya kuwakumbusha wanachama kujiandaa kupunguza uwekezaji kwa kujiandaa kuondoka na kwenda kwenye maisha mapya ambayo ni ya kuishi bila mshahara na uchumi pamoja na hadhi ndogo tofauti na sasa." Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka wastaafu hao watarajiwa kujiandaa na kuwa na uamuzi kwa kuwa na vitega uchumi kabla ya kustaafu na kupanga wapi wanakusudia kwenda kuishi kwani maisha ya mjini yanatofautiana na ya kijijini kwani yana asili tofauti ya mahitaji na aina ya biashara au shughuli za kuwekeza.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu NSSF nchini Robert Kadege ameshukuru uongozi wa Mkoa na Waajiri waliowaruhusu wastaafu 400 wataopata elimu ya juu ya kustaafu bila hofu, mafao na ukokotozi wa mafao pamoja na masuala ya afya kwa siku mbili.

Emanuel Kahensa, Meneja NSSF Mwanza ametumia wasaa huo kuwashukuru wanachama hao kwa uaminifu na kukubali kupata mafunzo hayo na akaahidi kuwapitisha kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wa namna gani wataenda kuishi kwa furaha baada ya kustaafu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.