• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI

Posted on: May 21st, 2025

RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Said Mtanda amesema uzinduzi wa wa Meli kubwa ya mizigo ya MV Mpungu yenye uwezo wa kubeba tani 1,000 sawa na magari ya kubeba mizigo (Trailer 21) ni ishara ya maendeleo na ukuaji wa sekta ya usafirishaji majini katika Mkoa wa Mwanza.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo mei 21,2025 wakati wa uzinduzi wa Meli hiyo ya MV Mpungu uliofanyika katika Bandari ya Mwanza Kusini ambapo amesema kuzindua meli hiyo katika Mkoa wa Mwanza ni uamuzi sahihi kwa kuwa ni Mkoa wa Kimkakati na kiuchumi.

“Ni matarajio ya wengi kuwa kuzindua kwa meli hii kubwa ya mizigo ya MV Mpungu itakata kiu ya Wafanyabiashara waliokuwa wakisubiri kwa hamu meli kubwa ya kusafirisha mizigo kutoka Mwanza kwenda Portbell, Uganda”. Amesema.

"Uwepo wa meli hii utachangia kukua kwa sekta ya usafirishaji majini na kukua kwa pato la Taifa." Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa amesema juhudi kubwa sana zimefanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuimarisha usafiri wa majini kwa ujenzi wa vivuko vitano (5) vyenye thamani ya Sh. Bilion 28.

Pia amesema serikali imetoa fedha takribani shilingi Bilioni 18.6 kugharamia mradi wa upanuzi wa Bandari ya Mwanza Kaskazini ambao umefikia Asilimia 58. Ujenzi wa Meli Mpya ya MV Mwanza itakayogharimu 123 Bilioni, yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo magari madogo 20 na malori 3, mradi umefikia asilimia 98.

“Lakini pia tuna ujenzi wa Makao Makuu ya Kituo cha Utafutaji na Uokozi katika Ukanda wa Ziwa Viktoria (MRCC –Regional Maritime Rescue Coordination Centre), unaogharimu 64.99 Bilioni na umefikia Asilimia 84”. Amefafanua.

Akisoma taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka za Bandari, Meneja wa Bandari Ziwa Victoria Bw. Erasto Ligenge amesema bandari ya Mwanz kusini ni moja ya vituo muhimu vya kimakakatu ambapo ina uwezo wa kuhudumia tani laki mbili kwa mwaka.

Aidha, amesema uzinduzi wa meli hiyo mpya ya mizigo itasaidia kubeba mizigo mingi kwa wakati mmoja ambapo kwa safari moja mizigo zaidi ya tani moja itasafirishwa kadhalika itapunguza safari za muda mrefu kwa njia ya barabara pamoja na kushusha wastani wa gharama za usafirishaji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI

    May 21, 2025
  • MSINGI WA MALEZI BORA KWA MTOTO UNAJENGA TAIFA IMARA: RC MTANDA

    May 21, 2025
  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.