• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza awataka Wananchi kuwaenzi Mashujaa wetu kwa uadilifu wa kulinda Rasilimali za Taifa

Posted on: July 25th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewaongoza Wananchi wa Mwanza katika kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa na kuwataka kuendelea kuwaenzi Mashujaa kwa vitendo ikiwemo uadilifu wa kulinda rasilimali za Taifa.

Sherehe hizo zilizofanyika leo katikati ya Jiji la Mwanza eneo la mzunguko uliopo Mnara wa Mashujaa hao waliopigana Vita Kuu ya Kwanza na ya Pili ya Dunia, Mkuu huyo wa Mkoa amesema haitakuwa na maana kuwakumbuka Mashujaa hao huku Wananchi wakiwa hawana uzalendo na Taifa lao.

"Hawa Mashujaa wetu licha ya kupigana Vita hizo walitumia silaha duni dhidi ya Wakoloni waliokuwa na silaha za kisasa lakini walitambua  wanapigania Taifa lao hivyo walijitoa muhanga huu ni mfano unaotakiwa kuendelea kuigwa kwa sisi tulio hai" Mhe Gabriel.

Katika Sherehe hizo,  Mzee Bega Maliba mwenye Umri wa Miaka 104 ambaye ni askari wa zamani aliyepigana Vita kuu ya Pili ya Dunia, alikua kivutio kwenye sherehe hizo na alipewa heshma ya kuweka Shoka kwenye Mnara wa Mashujaa.

Askari huyo wa zamani anayeishi Wilayani Ukerewe amesema kilichowapa heshma na kufanya vizuri enzi zao ni nidhamu ya hali ya juu waliyokuwa nayo wakiwa jeshini.

Aidha, Mkuu Mkoa ameweka Mkuki na Ngao kwenye Mnara kama ishara ya kuwakumbuka Mashujaa hao huku Viongozi wengine wa Serikali, Dini, Vyombo vya Ulinzi na usalama pamoja na Mtemi wa Mwanza Aron Nyamilonda wakiweka mashada ya maua,Sime na silaha za jadi.

Sherehe za kumbukumbu ya Mashujaa Kitaifa zimefanyika Mkoani Dodoma zikiongozwa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan.

Mashujaa hao wanaokumbukwa kila Julai 25 wamepigana Vita kuu ya kwanza iliyoanza mwaka 1914 hadi 18 na Ile ya Pili iliyopiganwa kuanzia mwaka 1939 hadi 45.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TAMISEMI ilivyotumia Wiki ya Kitaifa ya Usalama Barabarani Mkoani Mwanza kwa kutoa huduma mbalimbali kwa jamii

    March 22, 2023
  • RC Malima ataka adhabu kali na marekebisho ya Sheria za barabarani dhidi ya wanaosababisha ajali kwa uzembe

    March 17, 2023
  • Tupo katika mchakato wa Katiba mpya-Mhe.Dkt.Ndumbaro

    March 17, 2023
  • Miaka miwili ya Rais Samia madarakani,Mwanza yajivunia kasi ya miradi ya maendeleo

    March 15, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.